Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Timoteo 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Umukumbuke Yesu Kristo aliyekuwa wa ukoo wa mufalme Daudi, na aliyefufuka sawa vile inavyotangazwa na Habari Njema hii ninayohubiri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Timoteo 2:8
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Mungu alimufufua, akimufungua toka vifungo vya lufu, kwa sababu haikuwezekana afungwe na lufu.


Hiyo ndiyo itakayotokea siku ile Mungu atakapohukumu mambo ya siri ya watu kwa njia ya Yesu Kristo, kama vile Habari Njema yangu inavyosema.


Mungu amewaalika kuwa vile kwa njia ya Habari Njema tuliyowatangazia, kusudi mupate kushiriki katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.


Haya ni majina ya babu za Yesu Kristo, wa uzao wa Daudi, wa uzao wa Abrahamu. Abrahamu alizaa Isaka, Isaka alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yuda na wandugu zake, Yuda alizaa Peresi na Zera kutoka muke wake Tamari, Peresi alizaa Hesironi, Hesironi alizaa Ramu, Ramu alizaa Aminadabu, Aminadabu alizaa Nasoni, Nasoni alizaa Salmoni, Salmoni alizaa Boazi kutoka muke wake Rahaba, Boazi alizaa Obedi kutoka muke wake Ruta, Obedi alizaa Yese, Yese alizaa mufalme Daudi, Daudi alizaa Solomono (mama yake ndiye yule aliyekuwa muke wa marehemu Uria), Solomono alizaa Rehoboamu, Rehoboamu alizaa Abiya, Abiya alizaa Asa, Asa alizaa Yosafati, Yosafati alizaa Yoramu, Yoramu alizaa Uzia, Uzia alizaa Yotamu, Yotamu alizaa Ahazi, Ahazi alizaa Hezekia, Hezekia alizaa Manase, Manase alizaa Amoni, Amoni alizaa Yosia, Yosia alizaa Yekonia na wandugu zake, wakati Waisraeli walipohamishwa kwenda Babeli. Nyuma ya kuhamishwa kwa Waisraeli kwenda Babeli, Yekonia alizaa Saltieli, Saltieli alizaa Zerubabeli, Zerubabeli alizaa Abihudi, Abihudi alizaa Eliakimu, Eliakimu alizaa Azoro, Azoro alizaa Zadoki, Zadoki alizaa Akimu, Akimu alizaa Elihudi, Elihudi alizaa Eleazari, Eleazari alizaa Matani, Matani alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yosefu, yule alikuwa mume wa Maria, mama ya Yesu, anayeitwa Kristo.


Ni kwa hiyo nimewekwa kuwa mujumbe na mutume kwa kuwafundisha watu wa mataifa mengine kusudi wapate kumwamini Mungu na kutambua ukweli. Mimi ninasema ukweli wala si uongo.


Alizikwa na kufufuliwa kwa siku ya tatu kisha kufa kwake kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema.


Basi mumoja kati ya wale wazee akaniambia: “Usilie. Angalia, simba wa kabila la Yuda, wa uzao wa mufalme Daudi, amepata ushindi. Yeye anaweza kuvunja vile vifundo saba vya muhuri vya kizingo na kukifungua.”


Mafundisho haya yanalingana na Habari Njema ya utukufu wa Mungu mwenye baraka, ambayo nilipewa nipate kuihuburi.


Wandugu zangu, sasa ninataka kuwakumbusha Habari Njema niliyowatangazia, ile muliyopokea na kuishika imara.


Mungu asifiwe! Yeye yuko na uwezo wa kuwaimarisha katika imani juu ya Habari Njema ninayotangaza kwa kuhubiri ujumbe juu ya Yesu Kristo, kufuatana na ufunuo wa siri iliyofichwa tangia zamani za kale na kale.


Na toka katika uzao wa mutu huyo Mungu akawaletea Waisraeli Mwokozi, ndiye Kristo, kama vile alivyokuwa amewaahidia.


Lakini kwa sababu alikuwa nabii, alijua kwamba Mungu amemwahidi kwa kiapo kwamba atamutawalisha mumoja wa wazao wake kwa kurizi ufalme wake.


akiwaambia: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Kristo atateswa na kufufuka kwa siku ya tatu kisha kufa kwake.


Basi, usisikie haya ya kutoa ushuhuda kwa ajili ya Bwana wetu, wala usisikie haya kwa sababu yangu mimi ninayekuwa katika kifungo kwa ajili yake. Lakini ushiriki nami katika mateso kwa ajili ya Habari Njema, kufuatana na uwezo unaopewa na Mungu.


Ufikiri juu ya maneno hayo ninayosema, kwa maana Bwana atakupa uwezo kwa kuyaelewa yote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ