Na mbegu zilizoanguka katika miiba ni mufano wa wale wanaosikia, lakini masumbuko, utajiri na raha ya dunia vinawasonga hata wanashindwa kutoa matunda yanayokomaa.
Lakini siku zote tunasema vile Mungu anavyotaka, kwa maana yeye aliamua kwamba tunastahili, akatupatia kazi ya kuhubiri Habari Njema yake. Sisi hatutafuti kuwapendeza watu, lakini tunataka kupendeza Mungu, anayejua siri za mioyo yetu.
Kufuatana na hayo, ikiwa watu wamekwisha kuponyoka kuishi katika machafuko ya dunia kwa njia ya kumujua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, nao wakiyarudilia tena na kutawaliwa nayo, hali yao ya mwisho itakuwa mbaya zaidi kuliko ile ya kwanza!