Nawe Ezra, kwa kutumia hekima Mungu wako aliyokupa, hiyo unayokuwa nayo, chagua wanasheria, na waamuzi watakaowaongoza wakaaji wote wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati ambao wanaishi kufuatana na Sheria ya Mungu wako. Na yule ambaye haijui Sheria hiyo, umufundishe.
nikamuchagua ndugu yangu Hanani kuwa mwangalizi wa Yerusalema akishirikiana na Hanania aliyekuwa jemadari wa waaskari walinzi wa munara katika Yerusalema; kwa sababu alikuwa mutu wa kutegemewa na anayemwogopa sana Mungu, hapakukuwa mwingine aliyelingana naye,
Nabii aliyeota ndoto, atangaze ndoto yake, lakini yule aliyefunuliwa ujumbe wangu autangaze kwa uaminifu. Kuna ulinganifu gani kati ya maganda na ngano? –Ni ujumbe wa Yawe.–
Ni kazi ya makuhani kuwafundisha watu maarifa ya kweli juu ya Mungu kusudi watu wawaendee kwa kujifunza mapenzi yangu kwao, maana makuhani ni wajumbe wa Yawe wa majeshi.
Kisha akawaambia: “Basi, kila mwalimu wa Sheria aliyefundishwa katika Ufalme wa mbinguni, anafanana na mwenye nyumba anayetwaa vitu vipya na vitu vya zamani pamoja toka katika akiba yake.”
Bwana akajibu: “Ni nani basi anayekuwa musimamizi mwaminifu na mwenye akili? Ni yule bwana wake aliyemuweka kwa kuwasimamia watumishi wake wengine na kumwamuru kuwapatia posho lao kwa wakati uliopangwa.
Lakini Mungu ashukuriwe, maana yeye ndiye anayetupatia ushindi siku zote katika ushirika wetu pamoja na Kristo. Anatutumia sisi kwa kutambulisha Kristo pahali pote kama vile harufu nzuri ya marasi inavyosambaa popote.
Timoteo mwana wangu, ninakupa agizo hili kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Maneno hayo ndiyo yatakayokuwezesha kupiga vita nzuri,
Kama ukiwaelezea waziwazi wandugu maneno hayo, utakuwa mutumishi mwema wa Kristo Yesu, mwenye kukulishwa kiroho na maneno ya imani na mafundisho mazuri uliyoshika kabisa.
Lakini wewe umefuata kabisa mufano wangu katika mafundisho yangu na mwenendo wangu, makusudi yangu, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, ungojevu wangu,
Kwa hiyo ilimupasa afanane na wandugu zake katika mambo yote, kusudi apate kuwa Kuhani Mukubwa anayekuwa mwenye huruma na mwaminifu katika kazi yake mbele ya Mungu, na kwa njia hiyo zambi za watu zisamehewe.
Kisha, nitajiinulia kuhani mwingine mwaminifu atakayefanya kulingana na yale yanayokuwa ndani ya moyo na akili yangu. Nitamujengea ukoo imara, naye atatumika siku zote mbele ya mufalme wangu muchaguliwa.