Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Timoteo 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ninamushukuru Mungu ambaye ninamutumikia kwa zamiri safi kama vile babu zangu walivyofanya, ninapokukumbuka siku zote katika maombi yangu usiku na muchana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Timoteo 1:3
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha akabaki mujane, hata akaeneza umri wa miaka makumi nane na mine. Alibaki katika hekalu, akitumikia Mungu usiku na muchana, akifunga kula chakula na kuomba.


“Mimi ni Muyuda, nimezaliwa Tarso, katika jimbo la Kilikia, lakini nililelewa katika muji huu wa Yerusalema. Mimi nilikuwa mwanafunzi wa Gamalieli, na alinifundisha namna ya kufuata kabisa Sheria ya babu zetu. Nikajitolea kabisa kwa kutumikia Mungu kama vile ninyi wote munavyofanya leo.


Paulo akawakazia macho wale washauri wa Baraza Kubwa na kusema: “Wandugu zangu, mpaka leo zamiri yangu hainihukumu juu ya kitu chochote kinachoelekea mwenendo wangu mbele ya Mungu.”


Lakini ninakubali mbele yako kwamba ninamutumikia Mungu wa babu zetu nikifuata Njia ile wanayosema kwamba ni ya uongo. Mimi ninaamini maneno yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria na katika vitabu vya manabii.


Kwa sababu hii ninajikaza siku zote kuishi maisha safi bila kuhukumiwa na zamiri yangu mbele ya Mungu na mbele ya watu.


“Wayuda wote wanajua maisha yangu tangu mwanzo wa ujana wangu. Wanajua namna nilivyoishi kati ya taifa langu katika Yerusalema.


Kwa maana usiku malaika wa Mungu, ninayekuwa mutu wake na ninayemwabudu, alinitokea


Ninasema ukweli kwa kuungana na Kristo. Na kwa uongozi wa Roho Mutakatifu zamiri yangu inanihakikishia kwamba sisemi uongo:


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Nami niliendelea vizuri sana katika dini ya Kiyuda kuwapita watu wote wengine wa kabila langu wenye umri wangu, nikijikaza sana kushika desturi za babu zetu.


mimi sichoki kumushukuru Mungu kwa ajili yenu. Ninawakumbuka katika maombi yangu.


Usiku na muchana tunamwomba Mungu kwa bidii sana kusudi atupatie njia ya kuweza kuwaona tena na kuwaongezea kile munachokosewa katika imani yenu.


ukichunga imani yako na kuwa na zamiri safi. Watu wamoja wamekataa kuwa na zamiri hata wamepoteza imani yao.


Shabaha ya agizo hilo ni kusudi kuwe upendo unaotokana na moyo safi na zamiri nzuri na imani ya kweli.


Mujane wa kweli asiyekuwa na mutu yeyote wa kumusaidia, anamutumainia Mungu, na kudumu kumutolea mahitaji yake na kumwomba muchana na usiku.


Ninakumbuka vilevile imani yako isiyokuwa ya udanganyifu, imani ile tate muzaa mama yako Loisi na mama yako Euniki waliyokuwa nayo. Ninajua hakika kwamba wewe vilevile uko nayo.


Tena, tangia utoto wako unajua Maandiko Matakatifu yanayoweza kukupatia hekima kusudi uokolewe kwa njia ya kumwamini Kristo Yesu.


Yesu Kristo ni yule yule, jana, leo na hata milele.


Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Yawe; kufanya hivyo itakuwa kumukosea Yawe. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ