Mufalme akamwuliza: “Mwana wa bwana wako yuko wapi?” Siba akamwambia mufalme: “Yeye amebaki Yerusalema kwa sababu anazani kwamba watu wa Israeli watamurudishia ufalme wa Saulo babu yake.”
Mufalme akamwambia Siba: “Basi, yale yaliyokuwa mali ya Mefiboseti sasa ni mali yako.” Siba akamwambia: “Ninashukuru, bwana wangu mufalme, nami ninaomba nipate kukubaliwa mbele yako siku zote.”
Maana, jamaa yote ya babu yangu walikuwa watu ambao wamestahili kuuawa mbele yako, bwana wangu mufalme. Lakini uliniweka mimi mutumishi wako kati ya wale wanaokula kwenye meza yako. Nina haki yoyote zaidi hata nikulilie mufalme?”
Katika kabila la Benjamina, kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyeitwa Kisi. Yeye alikuwa mwana wa Abieli, mujukuu wa Zerori, wa jamaa ya Bekorati mwana wa Afia wa kabila la Benjamina.