Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 9:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Daudi akamwambia: “Usiogope. Mimi nitakutendea mema kwa ajili ya baba yako Yonatani. Nitakurudishia yale mashamba yote yaliyokuwa ya babu yako Saulo. Nawe, utakula kwenye meza yangu siku zote.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 9:7
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walipoona wamepelekwa kwenye nyumba ya Yosefu, wakashikwa na hofu, wakasema wao kwa wao: “Tumeletwa huku kwa sababu ya ile feza tuliyorudishiwa katika mifuko yetu tulipokuja safari ya kwanza kusudi apate kisingizio cha kutushambulia kwa rafla na kutunyanganya punda wetu na kutufanya watumwa wake.”


Yule musimamizi akawajibu: “Musikuwe na wasiwasi, wala musiogope. Bila shaka Mungu wenu, Mungu wa baba yenu, ndiye aliyewarudishia feza katika mifuko yenu. Mimi nilipokea feza yenu.” Kisha akawaletea Simeoni, ndugu yao.


Nilikupa nyumba ya bwana wako na wake zake wakuwe wako, tena nikakupa watu wa Israeli na wa Yuda uwatawale. Na kama haya yangekuwa kidogo sana kwako ningekuongezea mara mbili zaidi ya hayo.


Sasa, amenisingizia kwako, ee bwana wangu mufalme. Lakini wewe, bwana wangu mufalme, uko kama malaika wa Mungu. Fanya sawa unavyotaka.


Maana, jamaa yote ya babu yangu walikuwa watu ambao wamestahili kuuawa mbele yako, bwana wangu mufalme. Lakini uliniweka mimi mutumishi wako kati ya wale wanaokula kwenye meza yako. Nina haki yoyote zaidi hata nikulilie mufalme?”


Barzilayi alikuwa muzee sana, mwenye umri wa miaka makumi nane. Naye Barzilayi alikuwa amemutunza mufalme alipokaa kule Mahanaimu, kwa sababu alikuwa tajiri sana.


Mufalme alimwacha Mefiboseti mwana wa Yonatani kwa sababu ya kiapo ambacho Daudi na Yonatani mwana wa Saulo walikuwa wamefanya kati yao kwa jina la Yawe.


Siku moja, Daudi aliuliza: “Hakuna hata mutu mumoja aliyebakia katika jamaa ya Saulo? Kama yuko, ningependa kumutendea mema kwa ajili ya Yonatani.”


Wewe, watoto wako na watumishi wako mutakuwa munamulimia Mefiboseti na mutamuletea mavuno kusudi mujukuu wa bwana wako akuwe na chakula siku zote. Lakini yeye atakula kwa meza yangu.” Wakati ule, Siba alikuwa na wana kumi na watano na watumishi makumi mbili.


Kisha, Siba akamwambia mufalme: “Mimi mutumishi wako, nitafanya yote kulingana na amri yako.” Basi, Mefiboseti akakuwa anapata chakula chake kwenye meza ya Daudi, kama vile mumoja wa watoto wa mufalme.


Kwa hiyo, Mefiboseti aliyekuwa kilema wa miguu yake yote akakuwa anaishi katika Yerusalema, na kupata chakula chake kwenye meza ya mufalme siku zote.


Mufalme akamwuliza: “Hakuna hata mutu mumoja aliyebaki katika jamaa ya Saulo? Kama yuko, ningependa kumutendea wema wa Mungu.” Siba akamujibu: “Kuko mwana wa Yonatani. Yeye ni kilema.”


“Lakini uwatendee mema wana wa Barzilayi, yule Mugileadi, wakuwe kati ya wale wanaokula kwenye meza yako, kwa sababu walinitendea mema wakati nilipomukimbia ndugu yako Abusaloma.


Basi, Yoyakini akabadilisha nguo zake za mufungwa. Kila siku alikuwa anapata chakula chake kwa mufalme siku zote za maisha yake.


Wanasema: “Magonjwa haya yatamwua; hatatoka tena ndani ya kitanda chake!”


Basi, Yoyakinu alibadilisha nguo zake za wafungwa, akakuwa anapata chakula chake siku zote kwenye meza ya mufalme.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoe hukumu kwa haki, mutende mema na kuwa na huruma ninyi kwa ninyi.


kusudi mupate kula na kunywa pamoja nami katika ufalme wangu. Mutaikaa vilevile juu ya viti vya kifalme, kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.”


Sikiliza, ninasimama kwenye mulango na ninapiga hodi. Kama mutu akisikia sauti yangu na kunifungulia, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye atakula pamoja nami.


Basi, ninyi mumutii Yawe na kumutumikia kwa uaminifu, kwa moyo wenu wote. Mukumbuke yale mambo makubwa aliyowatendea.


tena usiache kuitendea jamaa yangu kwa uaminifu milele. Na Yawe atakapowateketeza waadui zako kutoka katika dunia,


Wewe, ukae pamoja nami, wala usiogope. Maana, anayetafuta kuyaangamiza maisha yangu anatafuta hata yako vilevile. Ukiwa pamoja nami, uko salama kabisa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ