2 Samweli 9:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20023 Mufalme akamwuliza: “Hakuna hata mutu mumoja aliyebaki katika jamaa ya Saulo? Kama yuko, ningependa kumutendea wema wa Mungu.” Siba akamujibu: “Kuko mwana wa Yonatani. Yeye ni kilema.” အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Yonatani mwana wa Saulo alikuwa na mutoto aliyekuwa kilema wa miguu. Mutoto huyo aliitwa Mefiboseti. Mefiboseti alikuwa na umri wa miaka mitano wakati habari za kifo cha Saulo na Yonatani ziliposikilika kutoka Yezereheli. Kwa wakati ule, mulezi wake aliposikia kwamba Saulo na Yonatani waliuawa kule Yezereheli, akamukamata Mefiboseti na kukimbia naye. Lakini alipokuwa anakimbia kwa haraka, mutoto huyo alianguka na kuwa kilema.