Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 9:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Wewe, watoto wako na watumishi wako mutakuwa munamulimia Mefiboseti na mutamuletea mavuno kusudi mujukuu wa bwana wako akuwe na chakula siku zote. Lakini yeye atakula kwa meza yangu.” Wakati ule, Siba alikuwa na wana kumi na watano na watumishi makumi mbili.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 9:10
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme akamwuliza: “Mwana wa bwana wako yuko wapi?” Siba akamwambia mufalme: “Yeye amebaki Yerusalema kwa sababu anazani kwamba watu wa Israeli watamurudishia ufalme wa Saulo babu yake.”


Simei alikwenda pamoja na watu wa kabila la Benjamina elfu moja. Siba mutumishi wa jamaa ya Saulo, pamoja na watoto wake kumi na watumishi makumi mbili, walikwenda haraka kwenye muto Yordani kumutangulia mufalme Daudi.


Sasa, amenisingizia kwako, ee bwana wangu mufalme. Lakini wewe, bwana wangu mufalme, uko kama malaika wa Mungu. Fanya sawa unavyotaka.


Mufalme alimwacha Mefiboseti mwana wa Yonatani kwa sababu ya kiapo ambacho Daudi na Yonatani mwana wa Saulo walikuwa wamefanya kati yao kwa jina la Yawe.


Daudi akamwambia: “Usiogope. Mimi nitakutendea mema kwa ajili ya baba yako Yonatani. Nitakurudishia yale mashamba yote yaliyokuwa ya babu yako Saulo. Nawe, utakula kwenye meza yangu siku zote.”


“Lakini uwatendee mema wana wa Barzilayi, yule Mugileadi, wakuwe kati ya wale wanaokula kwenye meza yako, kwa sababu walinitendea mema wakati nilipomukimbia ndugu yako Abusaloma.


Basi, Yoyakini akabadilisha nguo zake za mufungwa. Kila siku alikuwa anapata chakula chake kwa mufalme siku zote za maisha yake.


Siku zote alipewa posho na mufalme wa Babeli kulingana na mahitaji yake ya kila siku, mpaka alipokufa.


Mutu mumoja kati ya wale waliokuwa wakiikaa kula pamoja na Yesu aliposikia maneno hayo, akamwambia: “Heri mutu atakayeshiriki kwa kula karamu katika Ufalme wa Mungu!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ