Daudi alichukua vilevile shaba nyingi sana kutoka muji wa Tibuhati na muji wa Kuni iliyokuwa miji ya Hadadezeri. Solomono alitumia shaba hiyo kwa kutengeneza nguzo na vyombo vya shaba.
Kwa juhudi kubwa, nimeiwekea akiba nyumba ya Yawe zaidi ya toni elfu tatu za zahabu, zaidi ya toni elfu moja za feza pamoja na shaba na chuma visivyoweza kupimwa maana ni vingi sana. Nimetayarisha mbao na mawe. Lakini utaweza kuongeza.
walitoa kwa ajili ya kazi za nyumba ya Mungu: toni mia moja makumi saba za zahabu, vikoroti elfu kumi vya zahabu, na zaidi ya toni mia tatu za feza, yapata toni mia sita za shaba, na zaidi ya toni elfu mia tatu za chuma.
Kutoka hapo utaendelea mpaka Berota na Sibraimu (unaokuwa kati ya Damasiki na Hamati), na mpaka muji wa Hazori-Hatikoni unaokuwa katika inchi ya Haurani.