Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 8:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Halafu Daudi aliweka kambi za waaskari katika muji wa Waaramu wa Damasiki. Basi, Waaramu wakakuwa watumishi wake na wakakuwa wanamulipa kodi. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 8:6
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha wafalme wote waliokuwa watumishi wa Hadadezeri walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli, walifanya mapatano ya amani na Israeli, nao wakakuwa watumishi wa Israeli. Hivyo Waaramu hawakusubutu kuwasaidia Waamoni tena.


Naye Daudi wakati ule alikuwa katika maficho, nalo kundi la Wafilistini lilikuwa katika muji Betelehemu.


Sasa, mulilete jambo hilo mbele ya watu kwa sababu Yawe alimwahidi Daudi hivi: ‘Kwa mukono wako wewe Daudi mutumishi wangu, nitawaokoa watu wangu Waisraeli kutoka Wafilistini na kutoka waadui zao wengine.’ ”


Naye Daudi akazidi kuwa na uwezo zaidi kwa sababu Yawe, Mungu wa majeshi, alikuwa pamoja naye.


Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye utukufu kama wakubwa wengine katika dunia.


Akaweka kambi za waaskari katika inchi ya Edomu yote. Nao Waedomu wote wa kule wakakuwa watumishi wake. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.


Kisha aliwashinda Wamoabu. Aliwapanga katika mistari mateka hao, na kuwalalisha chini. Aliamuru wale waliokuwa katika mistari miwili wauawe na wale wa mustari wa tatu waachwe wazima. Hivyo, Wamoabu wakakuwa watumishi wa Daudi na wakakuwa wanamulipa kodi.


Daudi alitwaa ngao za zahabu waaskari wa Hadadezeri walizobeba na kuzipeleka Yerusalema.


Kisha kufa kwa Ahabu, watu wa Moabu waliasi wasitawaliwe na Israeli.


Mambo mengine ya Yeroboamu, yote aliyofanya, vita alivyopigana kwa ushujaa, na jinsi alivyoikomboa Damasiki na Hamati na kuifanya mali ya Israeli, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.


Basi, Yawe alikuwa pamoja naye, na alimwezesha kwa kila jambo alilotenda. Alimwasi mufalme wa Asuria na kukataa kumutumikia.


Mufalme Mesha wa Moabu alikuwa mufugaji wa kondoo, na kila mwaka alilipa kodi kwa mufalme wa Israeli wana-kondoo elfu mia moja na manyoya ya kondoo wengine elfu mia moja.


Basi akaweka kambi za waaskari kule Edomu. Nao Waedomu wote wakakuwa watumishi wa Daudi. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.


Aliweka majeshi katika miji yote ya inchi ya Yuda yenye kuta, na katika maeneo mengine ya Yuda akaweka waaskari walinzi, na katika miji ya Efuraimu ambayo baba yake Asa aliiteka.


Ninamwambia Yawe: “Wewe ni Mungu wangu.” Usikilize, ee Yawe, sauti ya ombi langu.


Moabu ni kama bakuli langu la kunawia. Nitatupia Edomu kiatu changu kwa kuirizi. Nitapiga kelele la ushindi juu ya Filistia.”


Farasi anatayarishwa kwa vita, lakini ushindi unaletwa na Yawe.


Yonatani alishinda kambi ya waaskari ya Wafilistini kule Geba, na Wafilistini wote walisikia juu ya habari hiyo. Hivyo Saulo alipiga baragumu katika inchi yote, akatangaza, akisema: “Waebrania wasikie.”


Siku moja, Yonatani mwana wa mufalme Saulo alimwambia kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende ngambo kwenye kambi ya Wafilistini.” Lakini Yonatani hakumwambia baba yake.


Kulikuwa hofu kubwa katika kambi ya Wafilistini. Wote walianza kufazaika: waaskari katika kambi, watu katika mashamba kwenye kambi, hata na washambulizi. Inchi ilitetemeka. Hofu ilikuwa kubwa sana.


Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ