Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 8:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Daudi vilevile alimushinda Hadadezeri mwana wa Rehobu, mufalme wa Zoba. Daudi alipata ushindi huu wakati Hadadezeri alipokuwa katika njia kwenda kulirudisha eneo la muto Furati kuwa chini ya utawala wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 8:3
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku hiyo, Yawe akafanya agano na Abramu akisema: “Ninawapa wazao wako inchi hii, toka muto Nili wa Misri mpaka ule muto mukubwa wa Furati,


Lakini Waaramu walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli, walijikusanya pamoja.


Hadadezeri aliagiza Waaramu waliokuwa ngambo ya muto Furati waletwe, wapelekwe kule Helamu wakiongozwa na Sobaki, jemadari wa waaskari wa Hadadezeri.


Kisha wafalme wote waliokuwa watumishi wa Hadadezeri walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli, walifanya mapatano ya amani na Israeli, nao wakakuwa watumishi wa Israeli. Hivyo Waaramu hawakusubutu kuwasaidia Waamoni tena.


Waamoni walipoona kwamba wamemuchukiza Daudi, walijilipia waaskari wa miguu wa Waaramu elfu makumi mbili kutoka Beti-Rehobu na Zoba, waaskari elfu kumi na mbili kutoka Tobu, na mufalme Maka akiwa na waaskari elfu moja.


Igali mwana wa Natani wa inchi ya Zoba; Bani wa muji Gadi;


Daudi akamushinda vilevile Hadadezeri mufalme wa Zoba, inchi iliyokuwa karibu na Hamati, alifanya hivyo wakati alipokuwa akienda kujisimamishia nguzo ya ukumbusho kwenye sehemu za muto Furati.


Nyuma ya pale Solomono akaenda katika muji wa Hamati-Soba na kuuteka,


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo “Ushuhuda wa mayungiyungi.” Mashairi ya Daudi ya kufundisha yanayoelekea wakati alipopigana na Wasuria katika Mesopotamia na Zoba naye Yoabu aliporudi nyuma na kuwaua Waedomu elfu kumi na mbili katika bonde la Chumvi.


Atawale kutoka bahari hata bahari, kutoka muto Furati hata miisho ya dunia.


Mipaka ya inchi yenu itakuwa kutoka bahari Nyekundu mpaka bahari ya Mediteranea na kutoka jangwa mpaka muto Furati. Nitawatia wakaaji wa inchi ile katika mikono yenu, nanyi mutawafukuza wawaondokee.


Kila pahali mutakapokanyaga kwa miguu yenu patakuwa penu. Inchi yenu itaenea kutoka katika jangwa, upande wa kusini, mpaka kwenye milima ya Lebanoni upande wa kaskazini, na kutoka muto Furati upande wa mashariki, mpaka kwenye bahari ya Mediteranea upande wa magaribi.


Saulo alipokwisha kuwa mufalme wa Waisraeli, alipigana na waadui zake wote kila upande: Wamoabu, Waamoni, Waedomu, wafalme wa Zoba na Wafilistini. Kila mara alipopigana vita, alishinda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ