Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 8:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kisha aliwashinda Wamoabu. Aliwapanga katika mistari mateka hao, na kuwalalisha chini. Aliamuru wale waliokuwa katika mistari miwili wauawe na wale wa mustari wa tatu waachwe wazima. Hivyo, Wamoabu wakakuwa watumishi wa Daudi na wakakuwa wanamulipa kodi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 8:2
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu aliwakamata watu wa muji ule, akawaweka kwa kazi ya kutumikisha misumeno, sururu za chuma, mashoka ya chuma na kuwatumia kufanya kazi katika furu ya matofali. Hivi ndivyo alivyoitendea miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na watu wote walirudi Yerusalema.


Halafu Daudi aliweka kambi za waaskari katika muji wa Waaramu wa Damasiki. Basi, Waaramu wakakuwa watumishi wake na wakakuwa wanamulipa kodi. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.


Kisha kufa kwa Ahabu, watu wa Moabu waliasi wasitawaliwe na Israeli.


Mufalme Salmanaseri wa Asuria alimushambulia; naye Hoshea akakuwa mutumishi wake na kumulipa kodi.


Akawashinda Wamoabu vilevile, wakakuwa watumishi wake na wakakuwa wanalipa kodi.


Waamoni walimulipa kodi, na sifa zake zikaenea mpaka Misri, kwa sababu alipata nguvu.


Gileadi ni yangu na Manase ni yangu; Efuraimu ni kofia yangu ya chuma, na Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.


Waliposikia tu habari zangu, walinitii; wageni walinijia wakinyenyekea.


Moabu ni kama bakuli langu la kunawia. Nitatupia Edomu kiatu changu kwa kuirizi. Nitapiga kelele la ushindi juu ya Filistia.”


Mungu amesema kutoka pahali pake patakatifu: “Sasa kwa shangwe nitaigawanya inchi ya Sekemu; Bonde la Sukoti nitalipima sehemu sehemu.


Kweli, wanakubaliana kwa moyo moja, wanafanya mapatano juu yako:


Musimusikilize Hezekia, maana mufalme wa Asuria anasema: Mukuwe na amani nami na kujitoa kwangu. Kisha kila mumoja wenu ataweza kula matunda ya mizabibu yake mwenyewe na matunda ya tini yake mwenyewe na kunywa maji ya kisima chake mwenyewe,


Ninamwona atakayekuja, ninamwona, lakini hayuko karibu. Nyota itatokea kwa wazao wa Yakobo, atatokea mufalme kati ya Waisraeli. Kwa fimbo yake atapiga viongozi wa Wamoabu, atawaangamiza wazao wote wa Seti.


Lakini watu wengine wasiofaa kitu, walisema: “Mutu huyu anaweza kutuokoa?” Walimuzarau Saulo na hawakumupa zawadi yoyote. Lakini yeye hakukasirika.


Saulo alipokwisha kuwa mufalme wa Waisraeli, alipigana na waadui zake wote kila upande: Wamoabu, Waamoni, Waedomu, wafalme wa Zoba na Wafilistini. Kila mara alipopigana vita, alishinda.


Kutoka kule, Daudi alikwenda mpaka Misipa katika inchi ya Moabu. Akamwambia mufalme wa Moabu: “Tafazali, baba yangu na mama yangu wakae hapa kwako mpaka nijue Mungu atanifanyia nini.”


Basi, Daudi aliwaacha wazazi wake wakae na mufalme wa Moabu; nao wakakaa kwake kwa muda wote ambao Daudi alikuwa katika nafasi za makimbilio.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ