Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 8:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa kiongozi wa Wakereti na Wapeleti. Wana wa Daudi wakakuwa makuhani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 8:18
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watumishi wote wa mufalme, Wakereti wote, Wapeleti wote, pamoja na Wagati mia sita waliomufuata mufalme Daudi kutoka muji wa Gati waliondoka pamoja naye wakimutangulia.


Sasa Yoabu alikuwa jemadari wa waaskari wote wa Waisraeli. Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa jemadari wa Wakereti na Wapeleti.


Ira wa muji Yairi alikuwa vilevile kuhani wa Daudi.


Abisayi akatoka akiwa pamoja na Yoabu, Wakereti na Wapeleti pamoja na mashujaa wote. Hao wote waliondoka Yerusalema kwenda kumufuata Seba mwana wa Bikiri.


Basi, kuhani Zadoki, nabii Natani na Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti, wote walishuka, wakamupandisha Solomono kwenye nyumbu wa mufalme Daudi, na kumupeleka mpaka Gihoni.


Naye mufalme amemupeleka pamoja na kuhani Zadoki, nabii Natani, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti, nao wamemupandisha juu ya nyumbu wa mufalme.


Lakini kuhani Zadoki, Benaya mwana wa Yehoyada, nabii Natani na Simei, na Rei pamoja na walinzi wa Daudi, hawakumwunga Adonia mukono.


Halafu mufalme Solomono akatoa amri kwa Benaya mwana wa Yehoyada; naye akamwendea Adonia, akamwua.


Lakini katika mwaka wa saba Yehoyada alituma ujumbe na kuwakusanya wakubwa wa waaskari na walinzi. Akaamuru wamufikie katika nyumba ya Yawe, naye akafanya nao mapatano na kuwaapisha humo katika nyumba ya Yawe. Halafu akawaonyesha Yoasi mwana wa mufalme Ahazia.


Benaya mwana wa Yehoyada, kutoka muji wa Kabuseli, alikuwa askari shujaa ambaye alifanya mambo mengi ya ajabu. Aliua mashujaa wawili kutoka Moabu, na siku moja wakati wa baridi kali, akashuka na kuua simba ndani ya shimo.


na Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mwangalizi wa waaskari walinzi wa Daudi; wana wa Daudi walikuwa na vyeo vikubwa katika utawala wake.


basi, mimi Bwana wenu Yawe ninawaambia hivi: Nitanyoosha mukono juu ya Wafilistini kwa kuwaazibu; nitawaangamiza hao watu wa Kereti na wakaaji wa kandokando ya bahari.


Ole wenu wakaaji wa inchi za pembeni ya bahari, watu wanaoishi kule Krete! Yawe amesema juu yenu, enyi wakaaji wa Kanana, inchi ya Wafilistini: Mimi nitawaangamiza wala hakutabaki hata mukaaji mumoja!


Sisi tulishambulia Negebu ya Wakereti na eneo la Yuda pamoja na Negebu ya Kalebu. Muji wa Ziklagi tuliuteketeza kwa moto.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ