Kuhani Abiatari akatoka, hata na kuhani Zadoki akatoka pamoja na Walawi wote wakilibeba Sanduku la Agano la Mungu. Wakaliweka lile Sanduku la Mungu chini, mpaka watu wote walipopita kutoka Yerusalema.
Mufalme Daudi akatuma ujumbe kwa makuhani Zadoki na Abiatari: “Muwaambie wazee wa Yuda: ‘Kwa nini ninyi ndio mutakuwa wa mwisho kumurudisha mufalme katika nyumba yake? Maneno yote Waisraeli waliyosema yamenifikia mimi mufalme.
Yehoyada akatwaa sanduku na kutoboa tundu kwenye kifuniko chake, kisha akaliweka kwenye mazabahu upande wa kuume, mutu anapoingia katika nyumba ya Yawe. Nao makuhani waliokuwa wakichunga kwenye mulango waliweka ndani ya sanduku feza zote zilizotolewa katika nyumba ya Yawe.
Walipomwita mufalme Hezekia walipokelewa na Eliakimu mwana wa Hilkia ambaye alikuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna aliyekuwa mwandishi wa mufalme, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wa habari.
kwa kutolea Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto juu ya mazabahu ya sadaka za kuteketezwa kwa moto siku zote asubui na magaribi, kulingana na yote yaliyoandikwa katika sheria ambayo Yawe aliyowaamuru Waisraeli.
Basi, Baruku alisoma maneno ya Yeremia kutoka katika kile kitabu mbele ya watu wote, ndani ya nyumba ya Yawe, katika chumba cha Gemaria mwana wa Safanu aliyekuwa katibu. Chumba hicho kilikuwa katika baraza la juu, kwenye mulango mupya wa nyumba ya Yawe.
Lakini makuhani wa kabila la Lawi ambao ni wazao wa Zadoki walioendelesha kazi yangu katika pahali patakatifu pangu, wakati Waisraeli waliponiacha, hao ndio watakaoendelea kunitumikia na kuja mbele yangu kunitolea mafuta na damu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
Si aliingia ndani ya nyumba ya Mungu na kula mikate mitakatifu iliyotolewa kwa Mungu? Jambo hili lilifanyika wakati Abiatari alipokuwa Kuhani Mukubwa. Ni makuhani tu walioruhusiwa kula mikate ile, lakini Daudi alikula na kuwapa watu wake vilevile.”