Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 8:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Kwa hiyo, Daudi akatawala juu ya Israeli yote, naye akawahukumu watu wake wote kufuatana na haki na sheria.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 8:15
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abusaloma alimwambia: “Maneno yako ni ya haki kabisa. Lakini hakuna mutu yeyote aliyechaguliwa na mufalme kwa kukusikiliza.”


Sasa Yoabu alikuwa jemadari wa waaskari wote wa Waisraeli. Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa jemadari wa Wakereti na Wapeleti.


Basi, Abeneri akatuma wajumbe kwa Daudi kule Hebroni wamwambie: “Inchi hii ni mali ya nani? Fanya agano na mimi, nami nitakusaidia kuifanya Israeli yote ikuwe chini yako.”


Kule Hebroni, alitawala watu wa Yuda kwa muda wa miaka saba na miezi sita, na kule Yerusalema alitawala watu wa Israeli pamoja na Yuda kwa muda wa miaka makumi tatu na mitatu.


Akaweka kambi za waaskari katika inchi ya Edomu yote. Nao Waedomu wote wa kule wakakuwa watumishi wake. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.


Yoabu mwana wa Zeruya alikuwa jemadari wa makundi yake ya waaskari. Yosafati mwana wa Ahiludi alikuwa mwandishi wa habari za kifalme.


Asifiwe Yawe, Mungu wako, ambaye amependezwa nawe, akakuweka juu ya kiti cha kifalme cha Israeli! Kwa sababu Yawe anapenda Israeli milele, amekuweka wewe ukuwe mufalme, kusudi uimarishe haki na sheria ya Mungu.”


Solomono alikuwa mufalme wa inchi yote ya Israeli, na hawa ndio walikuwa wakubwa wa serikali yake wenye vyeo vya juu: Azariya mwana wa Zadoki alikuwa kuhani. Elihorefu na Ahiya, wana wa Sisa, walikuwa wakatibu. Yosafati mwana wa Ahiludi alikuwa mwandishi wa habari. Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa jemadari wa waaskari. Zadoki na Abiatari walikuwa makuhani. Azariya mwana wa Natani alikuwa mukubwa wa maliwali. Kuhani Zabudi mwana wa Natani alikuwa rafiki ya mufalme. Ahisari alikuwa mukubwa wa nyumba ya mufalme. Adoniramu mwana wa Abuda alikuwa musimamizi wa kazi za kulazimishwa.


Halafu Daudi akatawala juu ya Israeli yote. Aliimarisha haki na sheria ya Mungu kwa watu wote.


Nimefanya mambo mema na ya haki; usiniache katika makucha ya waadui zangu.


Atawale taifa lako kwa haki, na wamasikini wako kwa sheria yako.


Tunakushukuru, ee Mungu, tunakushukuru! Tunatangaza ukubwa wa jina lako na kueleza matendo yako makubwa.


Mukono wako unajaa nguvu, mukono wako una nguvu na umeshinda!


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Muchukie mabaya, mupende mazuri, na kudumisha sheria ya Mungu katika tribinali. Labda Yawe wa majeshi atawarehemu watu wa kabila la Yosefu waliobaki.


Lakini muache haki itiririke kama maji, usawa ukuwe kama muto usiokauka.


Kwa njia ya imani hawa walishinda inchi za wafalme, walitenda mambo ya haki na kupata yale Mungu aliyowaahidi. Walifunga vinywa vya simba,


Saulo alipokwisha kuwa mufalme wa Waisraeli, alipigana na waadui zake wote kila upande: Wamoabu, Waamoni, Waedomu, wafalme wa Zoba na Wafilistini. Kila mara alipopigana vita, alishinda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ