Waamoni walipoona kwamba Waaramu wamekimbia, nao vilevile walimukimbia Abisayi na kuingia katika muji. Yoabu akaacha kupigana na Waamoni, akarudi Yerusalema.
Kisha aliwashinda Wamoabu. Aliwapanga katika mistari mateka hao, na kuwalalisha chini. Aliamuru wale waliokuwa katika mistari miwili wauawe na wale wa mustari wa tatu waachwe wazima. Hivyo, Wamoabu wakakuwa watumishi wa Daudi na wakakuwa wanamulipa kodi.
Zawadi zile, mufalme Daudi alizitakasa kwa ajili ya Yawe pamoja na feza na zahabu aliyonyanganya kwa mataifa yote, kutoka kwa: Waedomu, Wamoabu, Waamoni, Wafilistini na Waamaleki.
Katika muda huo, Daudi na watu wake waliwashambulia Wagesuri, Wagirzi na Waamaleki, ambao walikuwa wenyeji wa inchi hiyo tangu zamani. Aliwashambulia katika inchi yao mpaka Suri, hata kwa mupaka na Misri.
Daudi aliwapiga tangu asubui mpaka siku ya pili magaribi. Hakuna mwanaume yeyote aliyeponyoka isipokuwa vijana mia ine ambao walipanda juu ya ngamia na kukimbia.