Kisha, mufalme akatoka, akaenda, akaikaa kwenye nafasi yake karibu na mulango. Watu wote walipoambiwa kwamba mufalme yuko kwenye mulango, wote walimwendea. Wakati ule, watu wote wa Israeli walikuwa wamekimbia, kila mumoja kwake.
Lakini Yoabu na Abisayi walimufuatilia Abeneri. Jua lilipokuwa linatua wakafika kwenye mulima Ama, unaokuwa upande wa mashariki ya Gia, katika barabara inayokwenda katika jangwa la Gibeoni.
Wafilistini waliposikia kwamba Daudi amepakwa mafuta kuwa mufalme wa Waisraeli, wote walitoka kwenda kumutafuta, lakini yeye alipata habari, akaingia ndani ya makimbilio.
Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye utukufu kama wakubwa wengine katika dunia.
walizimisha moto mukali, waliponyoka kuuawa kwa upanga. Walikuwa wazaifu, lakini wakapata nguvu; walikuwa shujaa katika vita na kushinda majeshi ya kigeni.