Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 7:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Tena, hakuna watu katika dunia ambao wanaweza kufananishwa na watu wako Waisraeli. Ulikwenda kuwakomboa kutoka Misri na miungu yake kusudi wakuwe watu wako. Ukawafanyia jina na kuwatendea mambo makubwa na ya ajabu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 7:23
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata umewaimarisha watu wako Waisraeli kwa ajili yako mwenyewe, kusudi wakuwe watu wako milele; nawe ee Yawe umekuwa Mungu wao.


Tena ni watu gani katika dunia ambao wanaweza kulinganishwa na watu wako Waisraeli? Hao ndio watu peke yao Mungu wao alikwenda kuwakomboa kusudi wakuwe watu wake. Ukajipatia sifa kwa kutenda mambo makubwa na ya ajabu pale ulipofukuza mataifa mbele ya watu wako ambao uliwakomboa kutoka Misri.


Watu wa Israeli ni watumishi wako na watu wako uliwakomboa kwa uwezo wako na mukono wako wenye nguvu.


maajabu katika inchi hiyo ya Hamu, na mambo ya kutisha katika bahari Nyekundu.


Aliwakomboa watu wake na kufanya nao agano la milele. Yeye ni mutakatifu na wa kutisha sana!


Watu watatangaza ukubwa wa matendo yako ya ajabu, nami nitatangaza ukubwa wako.


Lakini hakuyatendea hivyo mataifa; wao hawajui maagizo yake. Haleluia!


Heri mutu anayemutumainia Yawe, mutu asiyejiunga na watu wenye majivuno, watu waliopotoka kwa kuabudu miungu ya uongo.


Kwa mukono wako mwenyewe uliyafukuza mataifa, na mahali pao ukawaikalisha watu wako; uliyaazibu mataifa, na kuwafanikisha watu wako.


Heri wale unaowachagua na kuwaleta karibu, waishi katika kiwanja chako. Sisi tutatoshelewa na mazuri ya nyumba yako, mazuri ya hekalu lako takatifu.


Mumwambie Mungu: “Matendo yako ni ya ajabu! Kwa nguvu yako kubwa waadui zako wanaishiwa nguvu.


“Usiku ule, nitapita katika inchi ya Misri na kuwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri, watu na nyama. Nitaiazibu miungu yote ya Misri. Mimi ni Yawe.


Maana namna gani itajulikana kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako, mimi na watu wako kama usipokwenda pamoja nasi? Ukienda pamoja nasi itatufanya mimi na watu wako kuwa watu wa pekee kati ya watu wote katika dunia.


Nitawafanya kuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Ninyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika nira za Wamisri.


Ningalikwisha kukuangamiza wewe na watu wako kwa ugonjwa mukali, nanyi mungalikuwa mumekwisha kuangamia.


Lakini nimewaacha muishi kwa kuonyesha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kwamba mimi ni nani.


Katika inchi ya Misri ulifanya maajabu, ukatenda miujiza, na unaendelea kufanya hivyo mpaka leo kati ya Waisraeli na katika mataifa mengine vilevile, jambo ambalo limekufanya ujulikane kila nafasi.


Kwa maajabu na miujiza uliyowatisha nayo Wamisri, uliwatoa watu wako Misri kwa nguvu zako nyingi na uwezo wako mukubwa.


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa wanaoishi nao, hao walioona nikijijulisha kwa Waisraeli wakati wa kuwatoa katika inchi ya Misri.


Ndivyo watakavyotamka jina langu juu ya Waisraeli, nami nitawabariki.


Basi tumusifu Mungu kwa sababu ya utukufu wa neema yake aliyotujalia kwa njia ya Mwana wake mupendwa.


Yeye ni utukufu wenu. Yeye ni Mungu wenu ambaye amewatendea haya mambo makubwa na ya kutisha muliyoona kwa macho yenu wenyewe.


Mukumbuke kwamba ninyi mulikuwa watumwa huko Misri na Yawe, Mungu wenu, aliwakomboa; ndiyo maana leo ninawaamuru hivyo.


Heri yenu ninyi Waisraeli. Nani anayekuwa kama ninyi, watu muliookolewa na Yawe, ambaye ndiye ngao ya musaada wenu, na upanga unaowaletea ushindi! Waadui zenu watakuja wananyenyekea mbele yenu, nanyi mutawakanyaga chini.”


Nikamwomba Yawe, nikisema: Ee Yawe, usiwaangamize watu wako na urizi wako, watu uliowakomboa na kuwatoa katika inchi ya Misri kwa uwezo na nguvu yako kubwa.


Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.


Basi, Wakanana pamoja na wakaaji wote wa inchi hii watakapopata habari hiyo watatuzunguka na kutufuta kabisa katika dunia. Sasa utafanya nini kwa kuonyesha ukubwa wa jina lako?”


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ