Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 7:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Kisha mufalme Daudi akaingia ndani na kuikaa mbele ya Yawe; halafu akaomba: “Mimi ni nani, ee Bwana wangu Yawe, na jamaa yangu ni nini hata ukaniinua mpaka hapa ninapokuwa leo!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 7:18
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Yakobo akamwomba Mungu akisema: “Ee Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu wa baba yangu Isaka! Ewe Yawe uliyeniambia nirudi katika inchi yangu kwa jamaa yangu, ukaniahidi kunitendea mema,


sistahili hata kidogo wema wote na uaminifu wote ulionitendea mimi mutumishi wako. Nilipovuka muto Yordani, sikukuwa na kitu isipokuwa fimbo; lakini sasa nina makundi haya mawili.


Hivi ndivyo jamaa yangu inavyokuwa mbele ya Mungu. Maana amefanya nami agano la kudumu milele; agano kamili na lenye kuwa imara. Naye atanifanikisha katika mahitaji yangu yote.


Natani alimwelezea Daudi kila kitu ambacho alionyeshwa katika maono hayo na Mungu.


Kisha mufalme Daudi akaingia ndani ya hema na kuikaa mbele ya Yawe, halafu akaomba: “Mimi ni nani, ee Yawe Mungu, na nyumba yangu ni nini hata unitukuze hivi?


“Lakini, mimi ni nani, na watu wangu ni nani, hata tuweze kutoa kwa mapenzi yetu hivi? Kwa maana vitu vyote vinatoka kwako, tumekutolea vitu vinavyokuwa vyako wewe mwenyewe.


Nikiangalia mbingu uliyoumba kwa vidole vyako, mwezi na nyota ulizozisimika huko,


Lakini Musa akamwambia Mungu: “Mimi ni nani hata nimwendee mufalme wa Misri na kuwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri?”


Mufalme Hezekia alipokea barua kutoka kwa wajumbe na kuisoma. Kisha akaenda na kuingia katika nyumba ya Yawe, akaiweka mbele ya Yawe.


Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


Gideoni akamujibu: “Tafazali Bwana, nitaweza namna gani kuikomboa Israeli? Ukoo wangu ndio wa bure zaidi katika kabila la Manase, na mimi mwenyewe ni mudogo kabisa katika jamaa yetu!”


Hapo Ruta akamwinamia Boazi uso mpaka chini kwa unyenyekevu, akamwambia: “Nimepata namna gani kukubaliwa mbele yako? Mbona unanishugulikia ijapokuwa mimi ni mugeni tu?”


Samweli akamwambia: “Ingawa unajiona kwamba wewe ni mudogo, lakini si wewe kiongozi wa makabila ya Israeli? Yawe alikupakaa mafuta kwa kukusimika kuwa mufalme juu ya Israeli.


Daudi akamwambia Saulo: “Mimi ni nani hata mufalme akuwe baba mukwe wangu? Ukoo wangu wenyewe na hata jamaa ya baba yangu si kitu katika Israeli.”


Saulo akajibu: “Mimi ni wa kabila la Benjamina, kabila dogo kuliko makabila yote ya Waisraeli. Na katika kabila lote la Benjamina jamaa yangu ndiyo ndogo kabisa. Lakini, kwa nini unanizungumuzia namna hiyo?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ