Hata hivyo, sitamunyanganya urizi wote, wala sitamwondolea mamlaka wakati angali anaishi, kwa ajili ya mutumishi wangu Daudi ambaye nilimuchagua, na ambaye alifuata amri zangu na masharti yangu.
Lakini wewe au watoto wako mukigeuka na kuacha kunifuata, musiposhika amri zangu na masharti niliyowapa, mukienda kutumikia miungu mingine na kuiabudu,
“Yawe aliniambia: ‘Mwana wako Solomono ndiye atakayenijengea nyumba na viwanja vyangu, kwa maana nimemuchagua yeye akuwe mwana wangu, nami nitakuwa baba yake.’
Maana mimi niko pamoja nawe, nipate kukuokoa. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitayaangamiza kabisa mataifa yote, ambayo niliyokusambaza kati yao; lakini sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakuazibu kadiri unavyostahili wala sitakuachilia uende bila kukuazibu. –Ni ujumbe wa Yawe.
Kwa maana Mungu hakumwambia hata mara moja mumoja wa wamalaika wake hivi: “Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.” Wala hakusema maneno haya juu ya malaika yeyote: “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwana wangu.”