Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 7:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 “Siku zako zitakapotimia na utakapokufa na kujiunga na babu zako, nitamufanya mumoja wa watoto wako wewe mwenyewe akuwe mufalme, nami nitauimarisha ufalme wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 7:12
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu neno la Yawe lilimufikia kusema hivi: “Huyu hatakuwa murizi wako! Mwana wako atakayetoka katika tumbo lako ndiye atakayekuwa murizi wako.”


Mungu anamujalia mufalme wake ushindi mukubwa; anamutendea mema muchaguliwa wake, ndiye Daudi na wazao wake milele.


Na kama sivyo, itatokea kwamba, wakati wewe bwana wangu mufalme utakapokufa, mimi pamoja na mwana wangu Solomono tutahesabiwa kama wenye kosa.”


na kuomba akisema: ‘Asifiwe Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye amemufanya muzao wangu kuwa mufalme kwa pahali pangu, na ambaye amenipa maisha hata nimeyaona mambo hayo.’ ”


Daudi alipokaribia kufa, alimwita mwana wake Solomono, akamupa maagizo akisema:


Naye Yawe atatimiza ahadi yake aliyotoa aliponiambia kwamba, ikiwa wazao wangu watatii amri zake na kumutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wote, hakutakosekana mumoja wao kwa kutawala Israeli nyakati zote.


Siku zote za utawala wake, watu wa Yuda na wa Israeli walikaa salama, kila mutu akistawi kwenye miti yake ya mizabibu na ya tini.


akasema: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli, maana kwa nguvu yake ametimiza ahadi yake aliyomupa baba yangu Daudi, akisema:


Hata hivyo, si wewe utakayenijengea nyumba, lakini ni mwana wako utakayemuzaa ndiye atakayenijengea hiyo nyumba.’


Na sasa, Yawe ametimiza ahadi yake, maana nimekuwa mufalme pahali pa baba yangu Daudi, na kukiikalia kiti cha kifalme cha Israeli kama vile Yawe alivyoahidi. Tena nimejenga nyumba ya kumwabudia Yawe, Mungu wa Israeli.


basi, mimi nitakiimarisha kiti chako cha kifalme juu ya Israeli milele, kama nilivyomwahidi baba yako Daudi, nikisema: Hautakosa mutu wa kuikaa juu ya kiti cha kifalme cha Israeli.


Lakini Yawe hakutaka kuangamiza Yuda, kwa sababu ya Daudi mutumishi wake, maana aliahidi kwamba wazao wake wataendelea kutawala milele.


Siku zako zitakapotimia za kujiunga na babu zako, nitamufanya mumoja wa watoto wako wewe mwenyewe akuwe mufalme; nami nitaimarisha ufalme wake.


Sasa, ee Mungu, Yawe, utimize ahadi uliyomupa Daudi baba yangu. Umeniweka kuwa mufalme juu ya watu hawa wanaokuwa wengi kama mavumbi.


Hamujui kwamba Yawe, Mungu wa Israeli, amemupa Daudi na wazao wake ufalme kwa milele kwa kufanya naye agano lisilovunjika?


lakini Yawe hakutaka kuangamiza ukoo wa Daudi kwa ajili ya agano alilokuwa amefanya na Daudi vilevile kwa sababu alikuwa ameahidi kwamba wazao wake wataendelea kutawala milele.


Mukutano wote ukafanya agano na mufalme katika nyumba ya Mungu. Yoyada akawaambia: “Muangalie huyu mwana wa mufalme! Mumwache atawale kulingana na ahadi Yawe aliyotoa juu ya uzao wa Daudi.


Umetimiza ahadi uliyotoa kwa mutumishi wako baba yangu Daudi, kweli, yale uliyosema umeyatimiza leo kwa uwezo wako mwenyewe.


Hata hivyo, si wewe utakayejenga nyumba, lakini mwana wako utakayemuzaa ndiye atakayenijengea ile nyumba.’ ”


Nitamwonyesha wema wangu kwa milele, na agano langu kwake litadumu siku zote.


Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Maana Yawe anasema hivi: Hakutakosekana hata kidogo mutu wa uzao wa Daudi atakayetawala Waisraeli.


Wengi wa wale ambao wamekwisha kufa, watafufuka; wengine watapata uzima wa milele, na wengine watapata haya na kuzarauliwa milele.


Haya ni majina ya babu za Yesu Kristo, wa uzao wa Daudi, wa uzao wa Abrahamu. Abrahamu alizaa Isaka, Isaka alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yuda na wandugu zake, Yuda alizaa Peresi na Zera kutoka muke wake Tamari, Peresi alizaa Hesironi, Hesironi alizaa Ramu, Ramu alizaa Aminadabu, Aminadabu alizaa Nasoni, Nasoni alizaa Salmoni, Salmoni alizaa Boazi kutoka muke wake Rahaba, Boazi alizaa Obedi kutoka muke wake Ruta, Obedi alizaa Yese, Yese alizaa mufalme Daudi, Daudi alizaa Solomono (mama yake ndiye yule aliyekuwa muke wa marehemu Uria), Solomono alizaa Rehoboamu, Rehoboamu alizaa Abiya, Abiya alizaa Asa, Asa alizaa Yosafati, Yosafati alizaa Yoramu, Yoramu alizaa Uzia, Uzia alizaa Yotamu, Yotamu alizaa Ahazi, Ahazi alizaa Hezekia, Hezekia alizaa Manase, Manase alizaa Amoni, Amoni alizaa Yosia, Yosia alizaa Yekonia na wandugu zake, wakati Waisraeli walipohamishwa kwenda Babeli. Nyuma ya kuhamishwa kwa Waisraeli kwenda Babeli, Yekonia alizaa Saltieli, Saltieli alizaa Zerubabeli, Zerubabeli alizaa Abihudi, Abihudi alizaa Eliakimu, Eliakimu alizaa Azoro, Azoro alizaa Zadoki, Zadoki alizaa Akimu, Akimu alizaa Elihudi, Elihudi alizaa Eleazari, Eleazari alizaa Matani, Matani alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yosefu, yule alikuwa mume wa Maria, mama ya Yesu, anayeitwa Kristo.


Yeye atakuwa mwenye mamlaka, na ataitwa Mwana wa Mungu Mukubwa. Bwana Mungu atamuweka kuwa mutawala wa ufalme wa babu yake Daudi.


Kisha akawaelezea maneno yaliyoandikwa juu yake katika Maandiko Matakatifu yote, akianza toka vitabu vya Musa na kuendelea katika vitabu vya manabii wote.


Lakini Daudi alipokwisha kutumika sawasawa na kusudi la Mungu katika maisha yake, akakufa na kwenda kukutana na babu zake waliomutangulia, naye akaoza.


Lakini kwa sababu alikuwa nabii, alijua kwamba Mungu amemwahidi kwa kiapo kwamba atamutawalisha mumoja wa wazao wake kwa kurizi ufalme wake.


Sasa nitawaambia ninyi siri: sisi wote hatutakufa, lakini sisi wote tutabadilishwa


Yawe akamwambia Musa: “Umekaribia sasa kuaga dunia, na kisha kufa kwako, watu wataanza kuniacha na kuendea miungu mingine ya inchi hiyo ambamo watakwenda kuishi. Wataniacha na kuvunja agano nililoagana nao.


Tunaamini kwamba Yesu alikufa na alifufuliwa, na kwa hiyo tunaamini vilevile kwamba Mungu atawafufua pamoja na Yesu wale waliokufa wakimwamini Yesu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ