Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 7:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Nami nitawachagulia watu wangu wa Israeli pahali pa kuishi niwapandikize kusudi waishi pahali pao wenyewe, wasisumbuliwe tena. Nao watu wakali hawatawatesa tena kama zamani,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 7:10
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na ikiwa Waisraeli watajali kutenda yote niliyowaamuru na kufuata sheria zote mutumishi wangu Musa alizowapa, basi sitawaacha wafukuzwe kutoka katika inchi hii ambayo niliwapa babu zao.”


Nami nitawachagulia watu wangu wa Israeli pahali pa kuishi niwapandikize, kusudi waishi pahali pao wenyewe, wasisumbuliwe tena. Nao watu wakali wanaotumia nguvu hawatawatesa tena kama zamani,


Na ikiwa watu wa Israeli watajali kutenda yote niliyowaamuru, Sheria yote, masharti, na maagizo yaliyotolewa kwa mukono wa Musa, basi sitawaacha hata kidogo wafukuzwe kutoka katika inchi hii ambayo niliwapa babu zao.”


Ee Mungu, sisi tumesikia kwa masikio yetu, babu zetu wametuelezea mambo uliyotenda nyakati zao, ndiyo mambo uliyotenda hapo kale.


Watu wako hawakuitwaa inchi kwa silaha zao, wala hawakupata ushindi kwa nguvu zao, lakini kwa mukono wako mwenyewe, kwa kuwaangazia uso wako, maana wewe uliwapenda.


Ee Mungu wa majeshi, utengeneze tena maisha yetu, utuangalie kwa wema, nasi tutaokoka.


Uliongoa muzabibu kutoka Misri; ukawafukuza watu wa mataifa, na kuupandikiza katika inchi yao.


Kisha mufalme wa Misri akawaamuru watu wake wote hivi: “Kila mutoto mwanaume atakayezaliwa kwa Waebrania mumutupe ndani ya muto Nili. Lakini kila mutoto mwanamuke, mumwache aishi.”


Wewe utawaleta watu wako na kuwapanda juu ya mulima wako, pale ulipochagua, ee Yawe, kuwa makao yako, pahali patakatifu, ee Yawe, ulipojenga kwa mikono yako.


Alililima vizuri na kuondoa mawe yote, akapanda humo mizabibu bora, alijenga munara wa ulinzi katikati yake, akachimba kikamulio cha divai. Kisha akatazamia lizae zabibu nzuri. Lakini likazaa zabibu chungu.


Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!


Mateso makali hayatasikilika tena katika inchi yako; wala uharibifu na maangamizi ndani ya mipaka yako. Utaweza kuziita kuta zako: “Wokovu”, na milango yako: “Sifa”.


Watu wako wote watakuwa wa haki, nao watarizi inchi milele. Hao ni chipukizi nililopanda mimi, kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.


Vilevile inaweza kunifikia kukusudia wakati wowote juu ya taifa au ufalme fulani kwamba nitalijenga na kulistawisha.


Nitawalinda siku zote na kuwarudisha katika inchi hii. Nitawajenga, wala sitawabomoa; nitawapanda, wala sitawaongoa.


Mungu anasema: Mataifa jirani za Waisraeli ambayo yalikuwa yanawauzi hayataweza tena kuwaumiza Waisraeli kama vile kwa miiba na michongoma. Halafu watajua kwamba mimi ni Bwana wao Yawe.


Siku hiyo, wewe utaniita “Mume wangu”, na sio tena “Bali wangu”. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nitawasimika katika inchi yao, wala hawataongolewa tena kutoka katika inchi niliyowapa. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Yeye atapanguza machozi yao yote na kifo hakitakuwa tena, wala kilio, wala malalamiko, wala maumivu. Kwa maana dunia ya mbele imekwisha kupita.”


Mufalme Asikie alikuwa na magari ya vita mia tisa ya chuma. Aliwagandamiza sana Waisraeli kwa miaka makumi mbili; nao wakamulilia Yawe awasaidie.


Wafilistini walitoka kwenye kambi yao kwenda kuwashambulia wakiwa katika vikundi vitatu. Kikundi kimoja kilielekea Ofura katika inchi ya Suali.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ