Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 7:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Wakati mufalme Daudi alipokuwa akikaa katika nyumba yake ya kifalme, naye Yawe amemwezesha kuwa na amani na waadui zake kila upande,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 7:1
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, mufalme Hiramu wa Tiro alituma wajumbe kwa Daudi. Alimupelekea vilevile miti ya mierezi, waseremala na wajengaji ambao walimujengea Daudi nyumba ya kifalme.


Basi Mikali binti ya Saulo hakukuwa na mutoto mpaka kufa kwake.


wakati nilipowachagua waamuzi juu ya watu wangu Waisraeli. Nami nitakulinda kutokana na waadui zako wote. Zaidi ya hayo, mimi Yawe ninakutangazia kwamba nitakujengea nyumba.


Inchi yote upande wa magaribi wa muto Furati, kutokea Tifusa mpaka muji wa Gaza, ilikuwa chini ya utawala wake. Wafalme wote upande wa magaribi wa muto Furati walikuwa chini yake, na alikuwa na amani na inchi zote jirani.


Halafu Daudi akamwita mwana wake Solomono, akamwagiza amujengee Yawe, Mungu wa Israeli, nyumba.


Daudi akamwambia Solomono: “Mwana wangu, nilikusudia ndani ya moyo wangu kumujengea Yawe, Mungu wangu, nyumba kwa kumutukuza.


Halafu mufalme Daudi akasimama na kusema: “Enyi wandugu zangu na watu wangu, munisikilize. Nilikusudia ndani ya moyo wangu kujenga nyumba kwa ajili ya Sanduku la Agano la Yawe, kiti cha kuwekea miguu ya Mungu wetu; na nilifanya matayarisho ya kujenga.


Naye Asa akawaambia watu wa Yuda: “Tujenge miji hii na kuizungushia kuta na minara, milango yenye vifungio vya vyuma. Inchi ingali katika mikono yetu kwa maana tumetenda mapenzi ya Yawe, Mungu wetu, naye ametupatia amani pande zote.” Basi wakajenga na kufanikiwa.


Basi, Yosafati akatawala kwa amani, na Mungu akamupa amani pande zote.


mpaka nikutayarishie wewe Yawe nafasi ya kukaa, ndiyo makao yako, ewe Mwenye Nguvu wa Yakobo!”


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi, mutumishi wa Mungu, aliyomwimbia wakati alipomwokoa katika mikono ya Saulo na waadui wengine.


Yawe akipendezwa na mwenendo wa mutu, anawageuza hata waadui zake kuwa warafiki.


Mara moja yule mutumishi aliyepata furushi tano, akaenda kufanya uchuuzi na mali ile, akafaidia zingine tano.


Mungu akamujalia Daudi neema hata akamwomba yeye Mungu wa Yakobo ruhusa ya kumujengea nyumba.


Yawe akawapa amani kila pahali katika inchi kama vile alivyowaapia wazee wao. Hakuna adui yeyote aliyesubutu kuwashambulia maana Yawe alikuwa amewatia waadui hao katika mikono yao.


Nyuma ya muda murefu, Yawe aliwajalia Waisraeli amani kwa kuwaokoa na waadui zao pande zote. Wakati ule Yoshua alikuwa muzee wa miaka mingi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ