Kisha, mufalme Hiramu wa Tiro alituma wajumbe kwa Daudi. Alimupelekea vilevile miti ya mierezi, waseremala na wajengaji ambao walimujengea Daudi nyumba ya kifalme.
wakati nilipowachagua waamuzi juu ya watu wangu Waisraeli. Nami nitakulinda kutokana na waadui zako wote. Zaidi ya hayo, mimi Yawe ninakutangazia kwamba nitakujengea nyumba.
Inchi yote upande wa magaribi wa muto Furati, kutokea Tifusa mpaka muji wa Gaza, ilikuwa chini ya utawala wake. Wafalme wote upande wa magaribi wa muto Furati walikuwa chini yake, na alikuwa na amani na inchi zote jirani.
Halafu mufalme Daudi akasimama na kusema: “Enyi wandugu zangu na watu wangu, munisikilize. Nilikusudia ndani ya moyo wangu kujenga nyumba kwa ajili ya Sanduku la Agano la Yawe, kiti cha kuwekea miguu ya Mungu wetu; na nilifanya matayarisho ya kujenga.
Naye Asa akawaambia watu wa Yuda: “Tujenge miji hii na kuizungushia kuta na minara, milango yenye vifungio vya vyuma. Inchi ingali katika mikono yetu kwa maana tumetenda mapenzi ya Yawe, Mungu wetu, naye ametupatia amani pande zote.” Basi wakajenga na kufanikiwa.
Yawe akawapa amani kila pahali katika inchi kama vile alivyowaapia wazee wao. Hakuna adui yeyote aliyesubutu kuwashambulia maana Yawe alikuwa amewatia waadui hao katika mikono yao.