Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 6:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Daudi aliporudi kwake kwa kuibariki jamaa yake, Mikali, binti ya Saulo, alikwenda kumupokea, akasema: “Ni ajabu kwa mufalme wa Waisraeli kujiheshimu leo, kwa kujifunua uchi wake mbele ya watumishi wake na wajakazi wake sawa vile mushenzi anavyovua nguo zake mbele ya watu bila haya!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 6:20
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nimemuchagua yeye na wazao wake. Yeye atawafundisha wazao wake kushika njia yangu kwa kutenda kwa haki na kwa kufuata sheria yangu, nami nitawatimizia ahadi zangu.”


Daudi alikuwa amejifungia kizibao cha kuhani katika kiuno chake. Alicheza kwa nguvu zake zote mbele ya Yawe.


Sanduku la Yawe lilipokuwa linaingia katika muji wa Daudi, Mikali binti wa Saulo alichungulia kwenye dirisha, akamwona mufalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele ya Yawe. Basi, akamuzarau ndani ya moyo wake.


Daudi alipomaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na za amani, aliwabariki watu kwa jina la Yawe wa majeshi,


na akawagawanyia watu wote, kundi lote la Waisraeli, wanaume na wanawake, kila mumoja, mukate, kipande cha nyama na mukate wa sadaka. Kisha, watu wote waliondoka, kila mutu akarudi kwake.


Kisha, kila mutu akaondoka kwenda kwake; naye Daudi akaenda kwake kwa kuibariki jamaa yake.


Walikuwa wapumbafu wakubwa na waovu ambao walilazimishwa kufukuzwa katika inchi kwa fimbo.


Nitashikamana na mwenendo mukamilifu. Utakuja kwangu wakati gani? Nitaishi kwa ukamilifu ndani ya nyumba yangu;


Mashairi yanayoelekea muzinduo wa hekalu. Zaburi ya Daudi.


Lakini vilevile, usikuwe mwovu sana wala usikuwe mupumbafu! Kwa nini kufa mbele ya wakati wako?


Petro alipokuwa angali chini ndani ya upango, mumoja wa watumishi wanawake wa Kuhani Mukubwa akafika pale.


Wandugu zake za jamaa waliposikia maneno haya, wakaondoka kwenda kumutwaa, kwa maana walisema kwamba amepotelewa na akili.


Alipofika kwenye Simoni Petro, Petro akamwambia: “Bwana, ni kweli wewe utaninawisha miguu?”


Kama hamutaki kumutumikia Yawe, basi muchague leo hii ni nani mutakayemutumikia: kama ni miungu ile ambayo wazee wenu waliitumikia ngambo ya muto Furati, au miungu ya Waamori ambao sasa munaishi katika inchi yao. Lakini mimi na jamaa yangu, tutamutumikia Yawe.”


Wakamupa vikoroti makumi saba vya feza vilivyokuwa kwenye nyumba ya Bali-Beriti ambavyo alivitumia kwa kulipa watu wakorofi na watu ovyoovyo kusudi wamufuate.


Wana wa Saulo walikuwa: Yonatani, Iswi na Malkisua. Wabinti zake walikuwa wawili; muzaliwa wa kwanza aliitwa Merabu na mudogo aliitwa Mikali.


Hata hivyo, Mikali binti mwingine wa Saulo alimupenda Daudi. Saulo alipoambiwa habari ile alifurahi sana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ