Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 6:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kisha waliliingiza Sanduku la Yawe ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha pale na kuliweka pahali pake. Naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele ya Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 6:17
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Solomono na mukutano wote wa Israeli wakakusanyika mbele ya Sanduku la Agano, nao wakatoa sadaka: ngombe na kondoo wasiohesabika.


Daudi akajengea nyumba katika muji wa Daudi. Tena akatengenezea Sanduku la Agano nafasi, akalipigia hema.


Basi, akawakusanya Waisraeli wote wakuje Yerusalema, kwa kuleta Sanduku la Agano la Yawe pahali alipolitayarishia.


Kisha wakaingiza Sanduku la Agano, na kuliweka ndani ya hema ambayo Daudi alikuwa ametayarisha. Halafu wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto na za amani mbele ya Mungu.


(Lakini, sanduku la Mungu lilikuwa Yerusalema katika hema ambalo mufalme Daudi alilipigia alipolileta kutoka Kiriati-Yearimu).


Mufalme Solomono na mukutano wa Waisraeli wakakusanyika mbele ya Sanduku la Agano nao wakatoa sadaka ya ngombe na kondoo wasiohesabika.


Simama sasa, ee Yawe, ukuje kwenye pumziko lako, pamoja na Sanduku la Agano la uwezo wako!


Kisha, kutoka katika sadaka hiyo ya amani Yawe anayotolewa kwa moto, atamutolea sehemu hizi: mafuta yake, mukia muzima wenye mafuta uliokatwa karibu kabisa na uti wa mugongo pamoja na mafuta yote yanayofunika matumbotumbo na mafuta yote yanayokuwa kwenye matumbotumbo,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ