Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 6:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Sanduku la Yawe lilipokuwa linaingia katika muji wa Daudi, Mikali binti wa Saulo alichungulia kwenye dirisha, akamwona mufalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele ya Yawe. Basi, akamuzarau ndani ya moyo wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 6:16
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi vilevile alituma wajumbe kwa Isiboseti mwana wa Saulo akisema: “Unirudishie muke wangu Mikali ambaye nilimwoa kwa magovi mia moja ya Wafilistini.”


Hata hivyo, mufalme Daudi aliteka kikingio cha Sayuni, ni kusema muji wa Daudi.


Hivyo, yeye na Waisraeli wote walilipeleka Sanduku la Yawe mpaka katika muji wa Daudi kwa shangwe na sauti kubwa ya baragumu.


Daudi aliporudi kwake kwa kuibariki jamaa yake, Mikali, binti ya Saulo, alikwenda kumupokea, akasema: “Ni ajabu kwa mufalme wa Waisraeli kujiheshimu leo, kwa kujifunua uchi wake mbele ya watumishi wake na wajakazi wake sawa vile mushenzi anavyovua nguo zake mbele ya watu bila haya!”


Sanduku la Agano la Yawe lilipokuwa likiingia katika muji wa Daudi, Mikali, binti wa Saulo, akachungulia kwenye dirisha, akamwona mufalme Daudi akicheza na kushangilia, basi akamuzarau ndani ya moyo wake.


Utuhurumie, ee Yawe, utuhurumie, maana tumezarauliwa kupita kipimo.


Wanaokutumainia wasifezeheke kwa sababu yangu, ee Bwana wetu, Yawe wa majeshi; wanaokutafuta, wasizarauliwe kwa sababu yangu, ee Mungu wa Israeli.


Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.


Lakini wengine waliwachekelea waamini, wakisema: “Watu hawa wamelewa kabisa.”


Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.


Saulo akamwambia Daudi: “Huyu ni Merabu, binti yangu mukubwa, nitamutoa kwako kusudi umwoe kwa masharti mawili: Ukuwe askari wangu shujaa na mutiifu, upigane vita ya Yawe.” Saulo alizani kwa njia hiyo Wafilistini watamwua Daudi, kusudi kitendo hicho asikifanye yeye mwenyewe.


Hata hivyo, Mikali binti mwingine wa Saulo alimupenda Daudi. Saulo alipoambiwa habari ile alifurahi sana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ