Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 6:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Mufalme Daudi aliposikia kwamba Yawe ameibariki jamaa ya Obedi-Edomu na vitu vyote alivyokuwa navyo kwa sababu ya Sanduku la Mungu, akaenda kuliondoa Sanduku la Agano kutoka katika nyumba ya Obedi-Edomu na kulipeleka kwenye muji wa Daudi kwa shangwe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 6:12
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, mufalme Daudi aliteka kikingio cha Sayuni, ni kusema muji wa Daudi.


Basi, mufalme Solomono akawakusanya mbele yake kule Yerusalema wazee na viongozi wote wa makabila na wa ukoo za Waisraeli kusudi waliondoe Sanduku la Agano la Yawe katika muji wa Daudi, ni kusema Sayuni.


Kisha kufika kwa wazee wote wa Israeli, makuhani walibeba Sanduku la Agano.


Walawi na makuhani walihamisha Sanduku la Agano na hema la mukutano, na vyombo vitakatifu vyote vilivyokuwa mule ndani ya hema.


Walawi wakalibeba juu ya mabega yao wakitumia miti yake ya kuibebea kama Musa alivyoamuru, kulingana na neno la Yawe.


Basi, Daudi, wazee wa Waisraeli na majemadari wa maelfu, wakaenda kutwaa Sanduku la Agano la Yawe kutoka katika nyumba ya Obedi-Edomu kwa shangwe.


Anashika agano alilofanya na Abrahamu, na ahadi aliyomwapia Isaka.


Vilevile kulikuwa Obedi-Edomu, ambaye Mungu alimubariki kwa kumupa wana wanane: Semaya muzaliwa wake wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa ine, Netaneli wa tano,


Amieli wa sita, Isakari wa saba na Peuletayi wa nane.


Basi mufalme Solomono akawakusanya kule Yerusalema wazee na viongozi wote wa makabila wa ukoo za Waisraeli kusudi waondoe Sanduku la Agano la Yawe kutoka katika muji wa Daudi, ni kusema Sayuni.


Na yeyote atakayetoa hata kikombe kimoja tu cha maji ya baridi kwa mumoja wa hao wanaokuwa wadogo kati ya wanafunzi wangu, kwa sababu yeye ni mwanafunzi wangu, kweli ninawaambia: mutu yule hatakosa kupewa zawadi yake.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ