Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 5:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme Daudi kule Hebroni. Naye akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Israeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 5:3
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wa Yuda walimwendea Daudi kule Hebroni wakamupakaa mafuta akuwe mufalme wao. Daudi aliposikia kwamba watu wa Yabesi-Gileadi ndio waliomuzika Saulo,


Lakini mukuwe imara na mashujaa. Saulo, bwana wenu, amekufa, na watu wa Yuda wamenipakaa mafuta nikuwe mufalme wao.”


Abeneri akamwambia Daudi: “Mimi sasa nitakwenda na kukuletea watu wote wa Israeli, wewe bwana wangu mufalme. Watakuja na kufanya agano nawe, kusudi ukuwe mufalme wao, nawe utawatawala wote kama unavyopenda.” Daudi akamwaga Abeneri aende zake, naye akaondoka kwa amani.


Halafu umuruhusu kuhani Zadoki na nabii Natani wamupakae mafuta akuwe mufalme wa Israeli. Kisha mupige baragumu na kusema: ‘Mufalme Solomono aishi!’


Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Yawe na mufalme na watu kwamba watakuwa watu wa Yawe. Vilevile alifanya agano kati ya mufalme na watu.


Kisha Waisraeli wote walikusanyika mbele ya Daudi kule Hebroni, wakamwambia: “Sisi ni mwili na damu yako.


Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme kule Hebroni; naye Daudi akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Waisraeli kulingana na neno la Yawe lililotolewa kwa njia ya Samweli.


Lakini Yawe, Mungu wa Israeli, alinichagua mimi kati ya jamaa ya baba yangu kuwa mufalme wa Israeli kwa milele. Alichagua kabila la Yuda kusudi liongozeke; na kutokana na kabila lile, alichagua jamaa ya baba yangu, na kati ya wana wa baba yangu, alipendezwa nami na kuniweka nikuwe mufalme wa Israeli yote.


Yoyada akafanya agano kati yake mwenyewe, watu wote, na mufalme kwamba watakuwa watu wa Yawe.


Kwenda uwakusanye wazee wa Israeli na kuwaambia kwamba: Yawe, Mungu wa babu wao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutokea na kusema: ‘Nimewachunguza ninyi na kuyaona mambo munayotendewa katika inchi ya Misri!


Halafu kutoka Eguloni Yoshua na Waisraeli wote wakaenda mpaka Hebroni, wakaushambulia


Yefuta akafuatana na wazee wa Gileadi, nao watu wakamufanya kiongozi wao. Yefuta akasema masharti yake kule Misipa mbele ya Yawe.


Watu wote wakaenda Gilgali, na walipofika kule, wakamusimika Saulo kuwa mufalme mbele ya Yawe. Wakamutolea Yawe sadaka za amani pale. Na Saulo pamoja na watu wote wa Israeli wakafurahi sana.


Samweli akatwaa pembe lake lenye mafuta akamupakaa Daudi mafuta mbele ya kaka zake. Mara moja roho wa Yawe akamushika Daudi kwa nguvu na kuwa naye tangu siku hiyo. Kisha Samweli akarudi katika muji wa Rama.


Hao wote wawili, wakafanya agano mbele ya Yawe. Daudi akabaki katika muji wa Horeshi na Yonatani akaenda zake kwenye nyumba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ