Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 5:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Zamani, Saulo alipokuwa mufalme wetu wewe ndiwe uliyewaongoza Waisraeli katika vita, na Yawe alikuambia: ‘Utakuwa muchungaji wa watu wangu Waisraeli; utakuwa mukubwa juu ya inchi ya Israeli.’ ”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 5:2
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini upinde wake bado imara, na mikono yake imepewa nguvu, kwa uwezo wa Mwenye Nguvu wa Yakobo, kwa jina la Muchungaji, Mulinzi wa Israeli.


Daudi akamwambia Mikali: “Nilikuwa mbele ya Yawe ambaye alinichagua mimi pahali pa baba yako na jamaa yake, kwa kunichagua kuwa mukubwa juu ya Waisraeli, watu wa Yawe. Kwa hiyo mimi nitacheza tu mbele ya Yawe.


Kila pahali ambako nimekwenda na Waisraeli wote, sikumwuliza mwamuzi yeyote wa Israeli ambaye nilimwamuru awachunge watu wa Israeli: ‘Kwa nini haujanijengea nyumba ya mierezi?’


Kwa hiyo basi, umwambie mutumishi wangu Daudi: Yawe wa majeshi anasema hivi: Nilikutoa katika shamba la malisho ya nyama ulimokuwa unawachunga kondoo, kusudi ukuwe mukubwa wa watu wangu Waisraeli.


“Rudi umwambie Hezekia, mukubwa wa watu wa Yawe, na kumwambia: Mimi, Yawe, Mungu wa babu yako Daudi, nimesikia ombi lako na nimeona machozi yako. Nitakuponyesha na nyuma ya siku tatu utaenda katika nyumba ya Yawe.


Zamani, Saulo alipokuwa mufalme wewe ndiwe uliyewaongoza Waisraeli katika vita, na Yawe, Mungu wako alikuambia: ‘Utakuwa muchungaji wa watu wangu Waisraeli, na utakuwa mukubwa wa watu wangu Waisraeli.’ ”


Kwa hiyo, ninakuomba unipe hekima na maarifa kusudi niweze kuwatawala watu wako vizuri. Kama sivyo, nitaweza namna gani kuwatawala hawa watu wako wanaokuwa wengi hivi?”


Atachunga kundi lake kama muchungaji, atawakusanya wana-kondoo katika mikono yake, atawabeba kwa kifua chake, na atawaongoza polepole kondoo wanaonyonyesha.


Mimi nilimufanya kuwa mukubwa na mutawala wa mataifa kusudi yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.


Nitaweka muchungaji mumoja juu yao, mufalme kama mutumishi wangu Daudi. Yeye atawakulisha na kuwa muchungaji wao.


Yeye ndiye atakayeleta amani. Waasuria wakishambulia inchi yetu, na kuingia katika nyumba zetu nzuri, tutatuma walinzi wetu wapigane nao, tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.


ambaye atawatangulia na kuwaongoza katika shuguli zao zote, kusudi wasikuwe kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.


‘Ewe Betelehemu, katika inchi ya Yuda, wewe si mudogo kabisa kati ya miji mikubwa ya Yuda, maana ndani yako atatoka mutawala, atakayechunga watu wangu, ndio Waisraeli.’ ”


“Mimi ni muchungaji mwema. Muchungaji mwema anatoa maisha yake kwa ajili ya kondoo wake.


Kwa hiyo ilifaa kwamba Mungu aliyeumba vitu vyote na kuvilinda imara, amufanye Yesu kuwa mukamilifu kwa njia ya mateso, kusudi awalete watoto wengi kuwa washiriki wa utukufu wa Mungu. Kwa maana Yesu ndiye anayewaongoza watu wapate kuokoka.


Lakini sasa ufalme wako hautadumu kwa sababu amri Yawe aliyokuamuru haukuitii. Yawe amejitafutia mutu mwingine ambaye atamutii kwa moyo wote, na huyo ndiye ambaye atamuchagua kuwa mutawala juu ya watu wake.”


Yawe akamwambia Samweli: “Utamulilia Saulo mpaka wakati gani? Wewe unajua kwamba mimi nimemukataa kuwa mufalme wa Israeli. Sasa, jaza ile pembe yako ya kuwekea mafuta, uondoke. Nitakutuma kwa Yese wa muji wa Betelehemu. Maana nimejipatia mufalme kati ya wana wake.”


Hivyo, Saulo akamwondoa na kumufanya kiongozi wa waaskari elfu moja. Naye Daudi akawaongoza vyema katika vita.


Lakini watu wote wa Israeli na Yuda walimupenda Daudi, maana ndiye aliwaongoza vizuri katika vita na kuwarudisha na mafanikio.


Kokote Daudi alikotumwa na Saulo, Daudi alifanikiwa. Hivyo, Saulo akamufanya kuwa mukubwa wa waaskari wake. Jambo hilo liliwafurahisha watu wote hata watumishi wa Saulo.


Ninakuomba unisamehe mimi mujakazi wako. Yawe atakupa jamaa imara kwa sababu, wewe bwana wangu, unapigana vita ya Yawe. Wakati wote wa maisha yako usipatikane na ubaya wowote.


Nyuma ya Yawe kukutendea mazuri yote aliyokuahidi, na kukuchagua kuwa mutawala wa Israeli,


“Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mutu kutoka inchi ya kabila la Benjamina, nawe utamupakaa mafuta kuwa mutawala wa watu wangu Waisraeli. Yeye atawaokoa watu wangu kutoka kwa Wafilistini, maana nimeyaona mateso ya watu wangu na kilio chao kimenifikia.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ