Katika mwaka wa kumi na ine, mufalme Kedorilaomeri na wale wafalme wenzake wakakuja na kuwashinda watu wa Refaimu kule Astaroti-Karnaimu, Wazuzi kule Hamu, Waemi kule Sawe-Kiriataimu,
Kisha, mashujaa watatu kati ya wakubwa makumi tatu waliteremuka wakati wa mavuno, wakamufikia Daudi kwenye pango kule Adulamu. Wakati ule kundi la waaskari wa Wafilistini lilikuwa limepiga kambi katika bonde la Refaimu.
Kisha mashujaa watatu kati ya wakubwa makumi tatu wakamwendea Daudi kwenye mulima wa pango la Adulamu. Wakati ule jeshi la Wafilistini lilikuwa limepiga kambi katika bonde la Refaimu.
Itakuwa kama wakati wa mavuno, wakati wamekwisha kuokota ngano, na kukusanya masuke katika mukono. Hakika, itakuwa kama bonde la Refaimu wakati wamekwisha kuvuna ngano.
Kisha, mupaka huo ulipitia kwenye Bonde la Hinomu, upande wa kusini wa kilima cha Wayebusi, ni kusema Yerusalema, kuelekea kilele cha mulima unaokuwa upande wa magaribi wa bonde la Hinomu na kufika mwisho wa bonde la Refaimu.
Yoshua akawajibu: “Kama mumekuwa wengi hivyo, hata inchi ya milima ya Efuraimu haiwatoshi tena, basi muende katika pori katika inchi ya Waperizi na ya Warefaimu, mufyeke pori hiyo na kufanya makao yenu kule.”
Kisha ulielekea chini kupitia pembeni ya mulima unaokuwa karibu na bonde la mwana wa Hinomu, ambalo lilikuwa katika sehemu ya kaskazini zaidi ya bonde la Warefaimu. Halafu mupaka uliteremuka kuelekea bonde la Hinomu, upande wa kusini wa kilima cha Wayebusi, ukaendelea kuteremuka mpaka Eni-Rogeli.