Kulikuwa vita ya muda murefu kati ya watu waliokuwa upande wa jamaa ya Saulo, na wale waliokuwa upande wa jamaa ya Daudi. Lakini Daudi alizidi kupata nguvu zaidi na zaidi, wakati upande wa Saulo ulizidi kuwa zaifu zaidi na zaidi.
Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye utukufu kama wakubwa wengine katika dunia.
Halafu Daudi aliweka kambi za waaskari katika muji wa Waaramu wa Damasiki. Basi, Waaramu wakakuwa watumishi wake na wakakuwa wanamulipa kodi. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.
Hata hivyo, ujipe moyo, ewe Zerubabeli. –Ni ujumbe wa Yawe. Ujipe moyo, Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki. Mujipe moyo nanyi watu wote wa inchi hii. –Ni ujumbe wa Yawe! Mufanye kazi, maana mimi niko pamoja nanyi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!
Kokote Daudi alikotumwa na Saulo, Daudi alifanikiwa. Hivyo, Saulo akamufanya kuwa mukubwa wa waaskari wake. Jambo hilo liliwafurahisha watu wote hata watumishi wa Saulo.