Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 5:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Naye Daudi akazidi kuwa na uwezo zaidi kwa sababu Yawe, Mungu wa majeshi, alikuwa pamoja naye.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 5:10
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati ule, Abimeleki pamoja na Fikoli, jemadari wa jeshi lake, akamwendea Abrahamu, akamwambia: “Mungu yuko pamoja nawe katika kila kitu unachofanya.


Kulikuwa vita ya muda murefu kati ya watu waliokuwa upande wa jamaa ya Saulo, na wale waliokuwa upande wa jamaa ya Daudi. Lakini Daudi alizidi kupata nguvu zaidi na zaidi, wakati upande wa Saulo ulizidi kuwa zaifu zaidi na zaidi.


Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye utukufu kama wakubwa wengine katika dunia.


Akaweka kambi za waaskari katika inchi ya Edomu yote. Nao Waedomu wote wa kule wakakuwa watumishi wake. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.


Halafu Daudi aliweka kambi za waaskari katika muji wa Waaramu wa Damasiki. Basi, Waaramu wakakuwa watumishi wake na wakakuwa wanamulipa kodi. Yawe alimupa Daudi ushindi kokote alikokwenda.


Hata hivyo, mutu wa haki anashika njia yake, mutu ambaye hajafanya ubaya kwa mukono wake anazidi kuwa na nguvu.


Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu? Ni Yawe, wa majeshi, yeye ndiye Mufalme mwenye utukufu.


Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu! Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote; mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!”


Mataifa yanakasirika na falme zinatikisika; Mungu ananguruma, nayo dunia inayeyuka.


Njia ya wenye haki ni kama mwangaza wa asubui mapema, ambao unaangaza zaidi na zaidi hata muchana kamili.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Hata hivyo, ujipe moyo, ewe Zerubabeli. –Ni ujumbe wa Yawe. Ujipe moyo, Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki. Mujipe moyo nanyi watu wote wa inchi hii. –Ni ujumbe wa Yawe! Mufanye kazi, maana mimi niko pamoja nanyi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!


Na Yesu alizidi kuwa na hekima, na kuongezeka kimo na kuendelea kumupendeza Mungu na watu.


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Saulo alikuwa anamwogopa Daudi kwa sababu Yawe alikuwa pamoja naye, lakini Yawe alikuwa amemwacha Saulo.


Daudi alifanikiwa katika kila kitu alichofanya, maana Yawe alikuwa pamoja naye.


Kokote Daudi alikotumwa na Saulo, Daudi alifanikiwa. Hivyo, Saulo akamufanya kuwa mukubwa wa waaskari wake. Jambo hilo liliwafurahisha watu wote hata watumishi wa Saulo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ