Mufalme Daudi akatuma ujumbe kwa makuhani Zadoki na Abiatari: “Muwaambie wazee wa Yuda: ‘Kwa nini ninyi ndio mutakuwa wa mwisho kumurudisha mufalme katika nyumba yake? Maneno yote Waisraeli waliyosema yamenifikia mimi mufalme.
Muulize vilevile Amasa kama yeye si damu yangu. Tena Mungu aniue ikiwa simufanyi yeye kuwa jemadari wa kundi langu la waaskari tangu leo pahali pa Yoabu.’ ”
Watu wa Yuda wakawaambia watu wa Israeli: “Kwa sababu mufalme ni ndugu yetu wa karibu. Kwa nini munakasirika juu ya jambo hili? Tumekula nini wakati wowote kutoka kwake? Au yeye ametupatia zawadi yoyote?”
Yoabu na watu wake walipeleka mwili wa Asaeli, wakauzika kwenye kaburi la baba yake, linalokuwa kule Betelehemu. Yoabu na watu wake walitembea usiku kucha, na kulipokucha wakafika katika muji wa Hebroni.
munaweza kumuweka mufalme juu yenu mutu ambaye Yawe, Mungu wenu, atamuchagua. Mutamuweka mumoja wa wandugu zenu kuwa mufalme juu yenu. Musimufanye mugeni asiyekuwa ndugu yenu kuwa mufalme wenu.
Basi kwa kuwa hao watoto ni wanadamu, wenye mwili na damu, Yesu vilevile alitwaa ile hali ya mwanadamu. Alifanya hivi kusudi kwa njia ya kufa kwake amwangamize Shetani aliyekuwa na uwezo wa kuleta lufu.
“Museme hapa hapa mbele ya wanainchi wote wa Sekemu: Jambo gani ni jema kwenu, kwamba watoto wote makumi saba wa kiume wa Yerubali wawatawale au mutoto mumoja? Mukumbuke kwamba mimi ni damu yenu.”