Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 4:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yonatani mwana wa Saulo alikuwa na mutoto aliyekuwa kilema wa miguu. Mutoto huyo aliitwa Mefiboseti. Mefiboseti alikuwa na umri wa miaka mitano wakati habari za kifo cha Saulo na Yonatani ziliposikilika kutoka Yezereheli. Kwa wakati ule, mulezi wake aliposikia kwamba Saulo na Yonatani waliuawa kule Yezereheli, akamukamata Mefiboseti na kukimbia naye. Lakini alipokuwa anakimbia kwa haraka, mutoto huyo alianguka na kuwa kilema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 4:4
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme alimwacha Mefiboseti mwana wa Yonatani kwa sababu ya kiapo ambacho Daudi na Yonatani mwana wa Saulo walikuwa wamefanya kati yao kwa jina la Yawe.


Kwa hiyo, Mefiboseti aliyekuwa kilema wa miguu yake yote akakuwa anaishi katika Yerusalema, na kupata chakula chake kwenye meza ya mufalme siku zote.


Mufalme akamwuliza: “Hakuna hata mutu mumoja aliyebaki katika jamaa ya Saulo? Kama yuko, ningependa kumutendea wema wa Mungu.” Siba akamujibu: “Kuko mwana wa Yonatani. Yeye ni kilema.”


Basi, Mefiboseti mwana wa Yonatani na mujukuu wa Saulo akaenda kwa mufalme Daudi, akainama uso mpaka chini mbele ya mufalme Daudi. Daudi akamwita: “Mefiboseti!” Naye akamujibu: “Ndiyo! Mimi mutumishi wako niko hapa.”


Lakini Hadadi ambaye wakati ule alikuwa kijana alitorokea Misri pamoja na Waedomu wamoja, watumishi wa baba yake.


Mwana wa Yonatani alikuwa: Meribu-Bali; Meribu-Bali alizaa Mika.


Yonatani alizaa Meribu-Bali, Meribu-Bali alizaa Mika.


Wafilistini walikusanya makundi yao yote ya waaskari kule Afeki, na Waisraeli walipiga kambi kwenye chemichemi ya bonde la Yezereheli.


Kwa hiyo, kesho yake asubui, Daudi pamoja na watu wake waliondoka kurudi katika inchi ya Wafilistini. Lakini hao Wafilistini wakaenda Yezereheli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ