Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mwana huyo wa Saulo alikuwa na watu wawili waliokuwa viongozi wa makundi yake ya waaskari. Mumoja aliitwa Bana na mwingine Rekabu. Hao walikuwa wana wa Rimoni, mutu wa kabila la Benjamina wa muji wa Beroti (kwa maana Beroti vilevile ulikuwa mali ya kabila la Benjamina).

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 4:2
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zeleki wa inchi ya Waamoni; Naharayi wa muji Beroti aliyekuwa mubebaji wa silaha wa Yoabu mwana wa Zeruya;


Kisha, Yoabu pamoja na watu wa Daudi walirudi kutoka kwenye mashambulio, wakaleta vitu vingi. Lakini Abeneri hakukuwa pamoja na Daudi kule Hebroni maana Daudi alikuwa amemwaga aende zake, naye akaondoka kwa amani.


Rekabu na Bana wana wa Rimoni wa Beroti wakaenda kwa nyumba ya Isiboseti. Walifika kule wakati wa jua kali ya muchana, Isiboseti alipokuwa anapumzika mwake.


Lakini Daudi akamujibu Rekabu na ndugu yake Bana, wana wa Rimoni wa Beroti: “Kama vile Yawe anavyoishi, yeye ameyakomboa maisha yangu kutoka kila adui.


Katika vita walivyokuwa wakipigana na Waisraeli, Waaramu walikuwa wamemukamata binti mumoja mudogo kutoka Israeli kuwa mufungwa, naye akakuwa anamutumikia muke wa Namani.


Mufalme wa Israeli akawafanyia karamu kubwa. Walipomaliza kula na kunywa, akawarudisha kwa bwana wao. Toka wakati ule, Waaramu hawakuishambulia tena inchi ya Israeli.


Basi, Waisraeli wakafunga safari, nyuma ya siku ya tatu wakafika katika miji yao. Miji hiyo ilikuwa Gibeoni, Kefira, Beroti na Kiriati-Yearimu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ