Kulikuwa vita ya muda murefu kati ya watu waliokuwa upande wa jamaa ya Saulo, na wale waliokuwa upande wa jamaa ya Daudi. Lakini Daudi alizidi kupata nguvu zaidi na zaidi, wakati upande wa Saulo ulizidi kuwa zaifu zaidi na zaidi.
Halafu Yehu akaingia katika hekalu la Bali akifuatana na Yonadabu na kuwaambia waliokuwa ndani ya hekalu: “Muhakikishe kwamba wanaokuwa humu ndani ya hekalu ni wale wanaomwabudu Bali tu, na kwamba hakuna mutu yeyote anayemwabudu Yawe.”
Lakini ukitaka kwenda, basi ufanye vile, ukuwe hodari katika vita, lakini Mungu atakufanya ushindwe na waadui, kwa maana Mungu ana nguvu kwa kusaidia au kumufanya mutu ashindwe.”