Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 3:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Kisha, watu wote walikwenda kumusihi Daudi akule chakula wakati ulipokuwa bado muchana. Lakini Daudi aliapa akawaambia: “Mungu aniue ikiwa nitaonja chakula au kitu chochote mpaka jua litakapotua.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 3:35
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakaomboleza, wakalia na kufunga kula mpaka magaribi kwa ajili ya Saulo, Yonatani mwana wake, na inchi ya Waisraeli, watu wa Yawe, kwa maana wengi kati yao waliuawa katika vita.


Wazee wa nyumba yake walimufuata na kumusihi aamuke, lakini yeye alikataa, na hakukula chakula chochote pamoja nao.


Mikono yako haikufungwa na miguu yako haikutiwa minyororo. Amekufa kama mutu aliyeuawa na waovu!” Na watu wote walimulilia tena.


Watu wote waliyaona mambo hayo, nao walipendezwa; kama vile kila kitu mufalme alichofanya kilivyowapendeza.


Mungu aniue ikiwa sitatimiza yote ambayo Yawe alimwapia Daudi.


mashujaa wote wakaondoka na kutwaa mwili wa Saulo na miili ya wana wake, wakaileta mpaka Yabesi. Wakazika mifupa yao chini ya muti wa mwalo kule Yabesi, nao wakafunga kula kwa muda wa siku saba.


Hakuna atakayechangia chakula na yule aliyekufiwa kwa kumufariji, wala kumupatia kinywaji cha kumufariji kwa ajili ya kukufiwa na mama au baba yake.


Utaugua, lakini sio kwa sauti. Hautamufanyia kilio huyo aliyekufa. Vaa viatu vyako na kuvaa kitambaa; usiufunike uso wako wala kula chakula cha kilio.


Ninyi mutafanya kama vile Ezekieli alivyofanya. Hamutazifunika nyuso zenu wala kula chakula cha kilio.


Basi Waisraeli wakaenda juu, wakamulilia Yawe mpaka magaribi. Kisha wakaomba shauri kwa Yawe: “Twende tena kupigana na wandugu zetu, wa kabila la Benjamina?” Yawe akawajibu: “Muende mupigane nao.”


Watu wote wa jeshi la Waisraeli wakaenda Beteli. Wakaikaa kule mbele ya Yawe wakiomboleza na kufunga mpaka magaribi. Wakamutolea Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani.


Pale utakapokufia ni pale nitakufia nami, na ni palepale nitazikwa. Yawe anipe azabu kali kama nikitenganishwa nawe isipokuwa tu kwa kifo.”


Eli akamwuliza: “Yawe alikuambia nini? Usinifiche alichokuambia. Ikiwa utanificha kitu alichokuambia, Mungu akuazibu vikali.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ