Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kiliabu muzaliwa wake wa pili, mama yake alikuwa Abigaili mujane wa Nabali wa muji wa Karmeli; Abusaloma muzaliwa wake wa tatu, mama yake alikuwa Maka binti ya Talmayi mufalme wa Gesuri;

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 3:3
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abusaloma mwana wa Daudi, alikuwa na dada yake muzuri sana aliyeitwa Tamari. Naye Amunoni, mwana mwingine wa Daudi, akamupenda sana Tamari.


Kwa hiyo, Yoabu aliondoka, akaenda Gesuri kumuleta Abusaloma katika Yerusalema.


Lakini mufalme akasema: “Abusaloma aishi kwake. Asikuje hapa kuniona.” Kwa hiyo, Abusaloma akakuwa anaishi mbali, kwake na hakumwona mufalme Daudi.


Abusaloma akamujibu: “Nilikutumia ujumbe, ukuje huku kusudi nikutume kwa mufalme, umwulize: ‘Kwa nini niliondoka Gesuri? Ingekuwa bora kwangu kubaki kule.’ Sasa unisaidie nipate kumwona mufalme. Kama nina kosa basi, aniue!”


Nyuma ya miaka mine, Abusaloma alimwambia mufalme: “Tafazali, uniruhusu niende kule Hebroni kwa kutimiza kiapo changu ambacho nilimwekea Yawe.


Maana, mimi mutumishi wako, nilipoishi kule Gesuri katika inchi ya Aramu, nilimufanyia Yawe kiapo nikisema kama Yawe akinirudisha Yerusalema basi, nitamwabudu yeye.”


Kwa hiyo Daudi alikwenda Hebroni, pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezereheli, na Abigaili, mujane wa Nabali, kutoka muji wa Karmeli.


Lakini baba yake Daudi hakukuwa amemukaripia mwana wake hata mara moja wala kumwuliza kwa nini alikuwa amefanya hivyo. Adonia alikuwa mwenye sura ya kupendeza sana na alikuwa amemufuata Abusaloma kwa kuzaliwa.


Adonia akamwambia: “Unajua kwamba ni mimi ndiye ningalikuwa mufalme, na hata Israeli yote ilikuwa inanitazamia nikuwe mufalme. Lakini, mambo yakageuka na ndugu yangu akanipindua, kwa sababu hayo ndiyo yaliyokuwa mapenzi ya Yawe.


Hawa ndio wana wa mufalme Daudi waliozaliwa wakati alipokuwa kule Hebroni: Amunoni, muzaliwa wake wa kwanza. Mama yake aliitwa Ahinoamu, wa muji wa Yezereheli; wa pili: Danieli ambaye mama yake aliitwa Abigaili wa muji wa Karmeli; wa tatu: Abusaloma, ambaye mama yake aliitwa Maka, binti ya Talmai mufalme wa Gesuri; wa ine: Adonia, ambaye mama yake aliitwa Hagiti; wa tano: Sefatia, ambaye mama yake aliitwa Abitali; wa sita: Itiramu, ambaye mama yake aliitwa Egla.


Yairi, mutu wa kabila la Manase, alitwaa eneo lote la inchi ya Argobu, ni kusema Basani, mpaka kwenye mupaka wa Gesuri na Maka. Vijiji vyote alivipa jina lake, na mpaka leo vinajulikana kama vile ‘Vijiji vya Yairi’.


Hata hivyo, Wagesuri na Wamakati hawakufukuzwa lakini wanaishi kati ya Waisraeli mpaka leo.


Mutu yule aliitwa Nabali na muke wake aliitwa Abigaili. Abigaili alikuwa mwanamuke mwenye akili na sura nzuri. Lakini Nabali alikuwa mutu wa chuki na mutenda maovu; tena alikuwa wa ukoo wa Kalebu.


Abigaili alifanya haraka, akasimama na kupanda juu ya punda wake, akifuatana na wajakazi wake watano, akaenda na watumishi wa Daudi. Akakuwa muke wake.


Katika muda huo, Daudi na watu wake waliwashambulia Wagesuri, Wagirzi na Waamaleki, ambao walikuwa wenyeji wa inchi hiyo tangu zamani. Aliwashambulia katika inchi yao mpaka Suri, hata kwa mupaka na Misri.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ