Daudi akasema: “Ubebe wewe mwenyewe lazima ya kifo chako, maana umejishuhudia wewe mwenyewe kwa kinywa chako mwenyewe ukisema: ‘Nimemwua muchaguliwa wa Yawe.’ ”
Yawe amekulipiza kisasi kutokana na kumwanga damu ya watu wote wa jamaa ya Saulo, ambaye sasa wewe umenyanganya ufalme kwa pahali pake. Sasa, Yawe amemupa mwana wako Abusaloma ufalme. Maangamizi yamekupata kwa sababu wewe ni mwuaji.”
Abeneri aliporudi Hebroni, Yoabu alimupeleka pembeni kwenye mulango sawa vile anataka kuzungumuza naye kwa siri. Hapo Yoabu akamukata Abeneri katika tumbo kwa sababu Abeneri alikuwa amemwua ndugu yake Asaeli, na Abeneri akakufa.
Lazima ya mauaji hayo yakuwe juu ya kichwa cha Yoabu na jamaa yote ya baba yake! Jamaa ya Yoabu isikose mutu mwenye ugonjwa wa kisonono siku zote, au ugonjwa wa ukoma, au anayetembelea kwa miti au kuuawa kwa upanga, au mwenye kukosa chakula!”
Mukifanya hivyo mutachafua inchi ambayo munakaa ndani yake. Umwangaji wa damu unachafua inchi, na hakuna sadaka inayoweza kutakasa inchi iliyofanyiwa mauaji isipokuwa kwa kumwua mwuaji huyo.
Basi Pilato alipoona kwamba hataweza kufanya kitu, isipokuwa tu kuongeza fujo, akatwaa maji na kunawa mikono yake mbele ya watu wote, akisema: “Lazima ya damu ya mutu huyu isikuwe juu ya kichwa changu! Maneno haya yanawaangukia.”