Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 3:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Abeneri aliporudi Hebroni, Yoabu alimupeleka pembeni kwenye mulango sawa vile anataka kuzungumuza naye kwa siri. Hapo Yoabu akamukata Abeneri katika tumbo kwa sababu Abeneri alikuwa amemwua ndugu yake Asaeli, na Abeneri akakufa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 3:27
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu, Abusaloma akamwambia: “Kama hauendi, basi, umuruhusu ndugu yangu Amunoni tuende naye.” Mufalme akamujibu: “Lakini kwa nini aende pamoja nanyi?”


Ninyi ni wandugu zangu, ninyi ni damu yangu. Kwa nini mukuwe wa mwisho kunirudisha mimi mufalme kwangu?


Yoabu alipotoka kuzungumuza na Daudi, alituma wajumbe wamulete Abeneri, nao wakamukuta kwenye kisima cha Sira na kumurudisha, lakini Daudi hakujua jambo hilo.


Nyuma ya pale Daudi aliposikia habari hizo alisema: “Mimi na ufalme wangu hatuna kosa mbele ya Yawe juu ya damu ya Abeneri mwana wa Neri.


Isiboseti mwana wa Saulo, aliposikia kwamba Abeneri ameuawa kule Hebroni, alivunjika moyo na watu wote wa Israeli walifazaika.


Mungu atamwazibu Yoabu kwa mauaji hayo aliyoyafanya bila baba yangu kuwa na habari. Yeye aliwaua watu wawili ambao walikuwa wa maana zaidi kuliko yeye, tena walimupita kwa wema; aliwaua Abeneri mwana wa Neri, jemadari wa kundi la waaskari Waisraeli, na Amasa mwana wa Yeteri, jemadari wa waaskari wa Yuda.


“Zaidi ya hayo, unajua vilevile yale Yoabu mwana wa Zeruya aliyonitendea, jinsi alivyowatendea majemadari wawili wa waaskari wa Israeli, Abeneri mwana wa Neri, na Amasa mwana wa Yeteri. Aliwaua wakati wa amani akitaka kulipiza kisasi kwa mauaji waliyofanya wakati wa vita. Aliwaua watu wasiokuwa na kosa, nami nikabeba lazima ya kifo cha watu wale kwa ajili ya vitendo vyake.


Anaweza kuficha chuki yake, lakini nia zake mbaya zitajulikana kwa wote.


Isimaeli mwana wa Netania pamoja na wale watu kumi, wakasimama na kumushambulia kwa upanga Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, wakamwua. Gedalia ndiye aliyekuwa amesimikwa na mufalme wa Babeli kuwa mutawala wa inchi.


Ndugu wa karibu wa mutu aliyeuawa atalipiza kisasi. Huyu atakapokutana na huyo mwuaji, atatimiza hukumu ya kifo.


Vilevile, kama mutu anamuchukia mwenzake halafu, akimusukuma au kumutupia kitu kwa kumuvizia,


“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayeua mutu kwa siri’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ