Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 3:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Lakini Paltieli akaenda pamoja na muke wake akiwa analia njia yote mpaka kule Bahurimu. Abeneri akamwambia Paltieli: “Rudia kwako.” Naye akarudi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 3:16
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Daudi alipofika kule Bahurimu, kulitokea mutu mumoja wa ukoo wa Saulo, jina lake Simei mwana wa Gera, akaanza kumulaani Daudi kwa mufululizo.


Lakini wakati huu, walionekana na kijana mumoja ambaye alikwenda na kumupasha Abusaloma habari. Kwa hiyo, Yonatani na Ahimasi waliondoka haraka, wakaenda Bahurimu katika nyumba ya mutu fulani aliyekuwa na kisima katika kiwanja chake. Wakaingia ndani ya kisima na kujificha.


Basi, mufalme akakuja kwenye muto Yordani na watu wote wa Yuda wakakuja mpaka Gilgali kwa kumupokea mufalme na kumuvukisha muto Yordani.


Simei mwana wa Gera, wa kabila la Benjamina, kutoka Bahurimu, alifanya haraka kwenda pamoja na watu wengine kwa kumupokea mufalme Daudi.


Abialboni wa muji Araba; Azimaweti wa muji Bahurimu;


Basi, Isiboseti alituma watu, wakamukamata Mikali kutoka kwa mume wake Paltieli mwana wa Laisi.


Vilevile, kuko Simei mwana wa Gera, wa kabila la Benjamina wa muji wa Bahurimu, ambaye aliniapiza na kunilaani vikali nilipokwenda kule Mahanaimu; lakini alipokuja kunipokea kwenye muto Yordani, nilimwapia kwa jina la Yawe nikimwambia: ‘Sitakuua kwa upanga.’


Isimaeli mwana wa Netania, alitoka inje ya muji kukutana na watu hao akiwa analia. Alipokutana nao, akawaambia: Karibu ndani ya nyumba kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ