Yawe alimwapia Daudi kwamba atauhamisha ufalme kutoka jamaa ya Saulo na kumupa yeye. Naye atatawala inchi ya Israeli na Yuda kutokea Dani mpaka Beri-Seba.”
Basi, Abeneri akatuma wajumbe kwa Daudi kule Hebroni wamwambie: “Inchi hii ni mali ya nani? Fanya agano na mimi, nami nitakusaidia kuifanya Israeli yote ikuwe chini yako.”