Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kulikuwa vita ya muda murefu kati ya watu waliokuwa upande wa jamaa ya Saulo, na wale waliokuwa upande wa jamaa ya Daudi. Lakini Daudi alizidi kupata nguvu zaidi na zaidi, wakati upande wa Saulo ulizidi kuwa zaifu zaidi na zaidi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 3:1
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


Vita ya siku hiyo ilikuwa kali. Abeneri na watu wa Israeli walipigwa vibaya na watu wa Daudi.


Kwa hiyo, Yoabu akapiga baragumu na watu wakaacha kuwafuatilia watu wa Israeli, wala hawakupigana zaidi.


Wewe uliniokoa na mashambulizi ya watu wangu, ukanichunga kuwa mutawala wa mataifa. Watu nisiowajua walinitumikia.


Kadiri vita ilivyoendelea kati ya jamaa ya Daudi na ile ya Saulo, Abeneri alizidi kujiimarisha katika jamaa ya Saulo.


Naye Daudi akazidi kuwa na uwezo zaidi kwa sababu Yawe, Mungu wa majeshi, alikuwa pamoja naye.


Siku zote kulikuwa vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.


Mufalme Asa wa Yuda na mufalme Basha wa Israeli walikuwa na vita kati yao wakati wote walipokuwa wakitawala.


Mufalme Asa wa Yuda na mufalme Basha wa Israeli walikuwa na vita kati yao wakati wote walipokuwa wakitawala.


Naye Daudi akazidi kuwa mukubwa kwa sababu Yawe wa majeshi alikuwa pamoja naye.


Hawa ndio wana wa mufalme Daudi waliozaliwa wakati alipokuwa kule Hebroni: Amunoni, muzaliwa wake wa kwanza. Mama yake aliitwa Ahinoamu, wa muji wa Yezereheli; wa pili: Danieli ambaye mama yake aliitwa Abigaili wa muji wa Karmeli; wa tatu: Abusaloma, ambaye mama yake aliitwa Maka, binti ya Talmai mufalme wa Gesuri; wa ine: Adonia, ambaye mama yake aliitwa Hagiti; wa tano: Sefatia, ambaye mama yake aliitwa Abitali; wa sita: Itiramu, ambaye mama yake aliitwa Egla.


Kule akawaelezea Zeresi, muke wake, na warafiki zake wote mambo yote yaliyomupata. Zeresi na hao warafiki zake wakamwambia: “Ikiwa huyu Mordekayi, ambaye umeanza kupoteza madaraka yako kwa ajili yake ni wa kabila la Wayuda, basi, hautamuweza; atakushinda kabisa.”


Mordekayi sasa akakuwa mutu mwenye madaraka makubwa katika nyumba ya kifalme, na habari zake zikaenea katika majimbo yote kwamba uwezo wake ulikuwa unazidi kuongezeka.


Hata hivyo, mutu wa haki anashika njia yake, mutu ambaye hajafanya ubaya kwa mukono wake anazidi kuwa na nguvu.


Na ingawa ulianza kuishi kwa uzaifu, maisha yako ya mwisho yatakuwa bora zaidi.


Niliwatwanga, wakakuwa kama vumbi inayopeperushwa na upepo; niliwakanyaga kama matope katika barabara.


Mukuje muone matendo ya Yawe. Muone maajabu aliyofanya katika dunia.


Wanapopita katika bonde lenye kukauka la Baka, wanalifanya kuwa chemichemi, nazo mvua za kwanza zinalijaza maji.


Kwa maana tamaa za kimwili zinapingana na tamaa za Roho Mutakatifu. Na tamaa za Roho zinapingana na tamaa za kimwili. Hao wawili wanapingana hata munashindwa kufanya sawa vile munavyotaka.


Kwa maana hatupigani na watu wa dunia hii, lakini tunapigana na pepo mbaya zinazokaa katika eneo la mbingu pamoja na wakubwa, na wenye mamlaka na watawala wa dunia hii ya giza.


Niliangalia, nami nikaona farasi mumoja mweupe. Na yule aliyepanda juu yake alikuwa na upindi, akapewa taji. Akatoka akiwa mushindaji na mwenye uwezo wa kuendelea kushinda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ