Yawe akawatia katika mikono ya Waisraeli, nao wakawashinda na kuwafukuza mpaka Sidona muji mukubwa na Misirepotaimu, mpaka upande wa mashariki katika bonde la Misipa. Waisraeli wakawapiga na kuwaua wote.
Watu wa kabila la Dani walipopoteza inchi yao, walikwenda na kuushambulia muji wa Lesemu. Waliushinda na kuuteka, na nyuma ya kuwaua wakaaji wake wote, wakaurizi halafu wakabadilisha jina la muji ule kuwa Dani; jina ambalo lilikuwa ni la babu yao.