Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 24:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Kisha Daudi akamujengea Yawe mazabahu pahali pale na kumutolea sadaka za kuteketezwa na za amani. Basi, Yawe akayakubali maombi kwa ajili ya inchi, na ule ugonjwa mukali uliowapata Waisraeli ikakoma.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 24:25
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yawe akamutokea Abramu, akamwambia: “Nitawapa wazao wako inchi hii.” Basi, Abramu akajenga mazabahu kwa ajili ya Yawe aliyemutokea.


Walipofika pahali ambapo Mungu alipomwagiza, Abrahamu akajenga mazabahu na kupanga kuni juu yake. Kisha akamufunga Isaka mwana wake na kumulalisha juu ya kuni kwenye mazabahu.


Noa akamujengea Yawe mazabahu, akatwaa mumoja katika kila aina ya nyama wanaohesabiwa kuwa safi na ndege anayehesabiwa kuwa safi, akamutolea Mungu sadaka za kuteketezwa kwa moto juu ya mazabahu.


Basi, watu wa Daudi wakaizika mifupa ya Saulo na ya mwana wake Yonatani katika inchi ya Benjamina, kule Zela katika kaburi la Kisi baba ya Saulo. Walifanya kila kitu ambacho mufalme aliamuru. Nyuma ya hayo, Yawe akayakubali maombi kwa ajili ya inchi.


Daudi akamujibu Gadi: “Nina mashaka makubwa! Lakini afazali kuazibiwa na Yawe, kuliko kutiwa katika mikono ya watu, maana yeye ana rehema sana.”


Wakati mufalme Daudi alipokuwa muzee sana, watumishi wake walimufunika kwa mablanketi, lakini, hata hivyo, hakuweza kupata joto.


Hivi, kasirani yangu itatosheka juu yako, wivu niliokuwa nao juu yako utakwisha; nitatulia wala sitaona hasira tena.


Alipofanya hivyo, pigo hilo likakoma, naye akabaki katikati ya waliokufa na waliokuwa wazima.


Kesho yake watu wakaamuka mapema, wakajenga mazabahu, wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani.


Gideoni akamujengea Yawe mazabahu kule na kuyaita, “Yawe ni Amani.” Mazabahu hiyo iko kule Ofura, muji wa Waabiezeri, mpaka leo.


Basi, Saulo akawaambia watu: “Muniletee sadaka yenu ya kuteketezwa na zile za amani.” Naye akatolea sadaka ya kuteketezwa.


Saulo akamujengea Yawe mazabahu. Hiyo ilikuwa ndiyo mazabahu ya kwanza ambayo Saulo alimujengea Yawe.


Kisha, alikuwa akirudi Rama, maana kule ndiko kulikuwa kwake. Aliwaamulia Waisraeli haki zao kule, na kumujengea Yawe mazabahu kule.


Kwa hiyo Samweli alitwaa mwana-kondoo anayenyonya akamutolea Yawe kama sadaka ya kuteketezwa. Kisha Samweli akamulilia Yawe kwa ajili ya Waisraeli, naye akajibu kilio chake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ