Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 24:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Kisha Arauna akamwuliza mufalme: “Kwa nini bwana wangu mufalme amenifikia mimi mutumishi wake?” Daudi akamujibu: “Nimekuja kununua kiwanja chako cha kupepetea ngano kusudi nimujengee Yawe mazabahu kusudi ugonjwa mukali uliowapata watu ukome.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 24:21
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walipofika katika uwanja wa kupepetea ngano wa Atadi, ngambo ya muto Yordani, waliomboleza kwa huzuni kubwa, naye Yosefu akamufanyia baba yake marehemu kilio cha siku saba.


Siku hiyo hiyo Gadi akamwendea Daudi, akamwambia: “Panda juu, umujengee Yawe mazabahu, katika kiwanja cha kupepetea ngano cha Arauna wa muji wa Yebusi.”


Arauna alipoangalia upande wa chini alimwona mufalme akimusogelea pamoja na watumishi wake, naye akatoka, akaenda na kuinama uso mpaka chini mbele ya mufalme.


Lakini Yoabu akamwambia mufalme: “Yawe, Mungu wako, awaongeze Waisraeli mara mia kuliko walivyokuwa sasa, nawe bwana wangu mufalme upate kuona ongezeko hilo kwa macho yako mwenyewe. Lakini, kwa nini wewe bwana wangu mufalme unapendezwa na jambo hili?”


Daudi akamwambia Ornani: “Unipe nafasi ya uwanja wako wa kupepetea ngano kusudi nimujengee Yawe mazabahu juu yake, kusudi ugonjwa mukali upate kuzuiliwa katika watu. Uniuzishie kwa bei yake kamili.”


Lakini Finehasi akasimama kutoa malipizi, na yale magonjwa yakakoma.


na kumufuatilia yule Mwisraeli mpaka ndani ya hema, akawachoma mukuki wote wawili ndani ya tumbo. Ugonjwa mukali uliokuwa umewaangamiza Waisraeli ukakomeshwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ