Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 24:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Lakini wakati malaika aliponyoosha mukono wake kuelekea Yerusalema kwa kuuangamiza, Yawe alibadilisha nia yake. Yawe akamwambia yule malaika aliyetimiza maangamizi kwa watu: “Basi! Inatosha; rudisha mukono wako.” Malaika wa Yawe alikuwa amesimama karibu na kiwanja cha kupepetea ngano cha Arauna wa muji wa Yebusi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 24:16
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

na vilevile babu ya Wayebusi, Waamori, Wagirgasi,


Yawe akasikitika sana kwa kumwumba mwanadamu katika dunia. Yawe akahuzunika sana ndani ya moyo wake.


Siku hiyo hiyo Gadi akamwendea Daudi, akamwambia: “Panda juu, umujengee Yawe mazabahu, katika kiwanja cha kupepetea ngano cha Arauna wa muji wa Yebusi.”


Siku hiyo, Daudi alisema: “Mutu yeyote atakayewapiga Wayebusi apitie kwenye mufereji wa maji kwa kuwashambulia vilema na vipofu ambao roho yangu inawachukia.” Ndiyo maana watu wanasema: “Vipofu na vilema hawataingia katika nyumba.”


naye akatembea mwendo wa siku nzima kuingia katika jangwa. Basi, akafika, akaikaa chini ya muti mumoja wa muretemu. Halafu, akaomba apate kufa, akisema: “Inatosha! Siwezi tena. Ee Yawe, sasa utoe uzima wangu. Mimi si bora kuliko babu zangu.”


Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


Kanana vilevile ndiye babu ya Wayebusi, Waamori, Wagirgasi,


Kisha Solomono akaanza kujenga nyumba ya Yawe katika Yerusalema juu ya mulima Moria ambapo Yawe alimutokea Daudi baba yake, pahali ambapo Daudi alikuwa amepachagua, kwenye kiwanja cha kupepetea ngano cha Ornani Muyebusi.


Naye Yawe akatuma malaika aliyewaua waaskari shujaa, majemadari na wakubwa katika kambi ya mufalme wa Asuria. Basi, mufalme wa Asuria akarudia katika inchi yake akijaa haya. Mara tu alipoingia ndani ya nyumba ya mungu wake, wana wake mwenyewe wakamwua palepale kwa upanga.


Yawe atawatetea watu wake; na kuwaonea huruma watumishi wake.


Njia yao ikuwe ya giza na utelezi, wakifukuzwa na malaika wa Yawe!


Lakini Mungu mwenye huruma alisamehe uovu wao, wala hakuwaangamiza. Mara nyingi alizuia hasira yake, wala hakuacha kasirani yake yote iwake.


Ee Yawe, urudie! Utakasirika mpaka wakati gani? Utuonee huruma sisi watumishi wako.


Basi, ile damu itakuwa kitambulisho chenu cha kuonyesha nyumba mutakamokuwa. Nami nitakapoiona ile damu, nitawapita ninyi, hamutapatwa na hasara yoyote wakati nitakapoipiga inchi ya Misri.


Maana Yawe atapita kuwaua Wamisri. Lakini atakapoona damu iliyopakwa kwenye vizingiti na miimo ya nyumba zenu, atapita na wala hatamuruhusu mwangamizaji kuingia katika nyumba zenu na kuwaua.


Basi, Yawe akaacha kuwafanyia watu wake lile jambo baya alilokuwa amesema.


Mumwombe Yawe maana ngurumo hii na mvua ya mawe vimezidi. Mimi nitawaacha muondoke na wala hamutabakia tena.”


Aliwaazibu watu wake kwa kuwapeleka katika uhamisho. Wakati wa upepo mukali wa mashariki, aliwaondoa kwa pigo kali.


Maana sitaendelea kugombana wala kuwakasirikia siku zote, maana hao niliowaumba watazimia mbele yangu, nami ndiye niliyewapa pumzi yangu ya uzima.


Hezekia, mufalme wa Yuda, na watu wote wa Yuda hawakumwua Mika. Hezekia alimwogopa Yawe na kuomba rehema kwake. Naye Yawe akabadilisha nia yake ya kuleta hasara aliyokusudia juu yao. Lakini sisi tuko mbio kwa kujiletea hasara wenyewe.


Kama ninyi mutabaki katika inchi hii, basi, nitawasimamisha, wala sitawaharibu; nitawaotesha wala sitawaongoa; kwa maana nitabadilisha nia kwa sababu ya hasara niliyowatendea.


Basi, Bwana wetu Yawe akabadilisha nia yake, akasema: Halitatukia!


Basi, Yawe akabadilisha nia yake, akasema: Hili vilevile halitatukia.


Ee Yawe, nimesikia juu ya utukufu wako, juu ya matendo yako, nami ninaogopa. Uyafanye tena mambo yale wakati wetu; uyafanye yajulikane wakati huu wetu. Unapokasirika tafazali ukumbuke huruma yako!


Nitawakomesha kula nyama yenye damu, na chakula ambacho ni chukizo. Watakaobaki watakuwa mali yangu, kama ukoo mumoja katika Yuda. Watu wa Ekroni watakuwa kama Wayebusi.


Aliporudi kwa mara ya tatu, akawaambia: “Mungali munalala na kupumzika? Inatosha! Saa imetimia. Sasa Mwana wa Mutu anatolewa katika mikono ya wenye zambi.


Na pale pale malaika wa Bwana akamwazibu Herode kwa ugonjwa kwa sababu alijitukuza kwa pahali pa Mungu. Herode akakuliwa na michango ya tumbo na kisha akakufa.


Musinungunike kama vile wamoja kati yao walivyofanya hata malaika mwangamizaji akawateketeza.


Azabu mutu yule aliyopewa na watu wengi kati yenu inatosha kwake.


Lakini watu wa Yuda hawakuweza kuwafukuza Wayebusi, ambao ndio waliokuwa wenyeji wa Yerusalema, na mpaka leo Wayebusi wangali wanaishi katika muji ule pamoja na watu wa Yuda.


Lakini watu wa kabila la Benjamina hawakuwafukuza Wayebusi waliokaa katika Yerusalema; ndiyo maana Wayebusi wanakaa pamoja na watu wa kabila la Benjamina katika Yerusalema mpaka leo.


Walipokuwa wanakaribia muji wa Yebusi, siku ilikuwa karibu imekwisha, naye mutumishi akamwambia bwana wake: “Sasa heri tuingie katika muji huu wa Wayebusi tulale mule usiku huu.”


“Ninajuta kwamba nimemufanya Saulo kuwa mufalme. Yeye ameacha kunifuata mimi na hajatimiza amri zangu.” Samweli alikasirika, akamulilia Yawe usiku kucha.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ