2 Samweli 24:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
15 Basi, Yawe akawaletea Waisraeli ugonjwa, tangu asubui mpaka wakati uliopangwa. Watu elfu makumi saba walikufa katika inchi yote kutoka Dani mpaka Beri-Seba.
Halafu, mufalme akamwambia Yoabu na majemadari wa kundi la waaskari waliokuwa pamoja naye: “Muzunguke katika makabila yote ya Waisraeli kutokea Dani mpaka Beri-Seba, muwahesabu watu kusudi nipate kujua jumla yao.”
Yoabu mwana wa Zeruya alianza kuwahesabu lakini hakumaliza; tena kasirani iliwapata Waisraeli kwa ajili ya tendo hili, nayo hesabu haikuingizwa katika kitabu cha habari za mufalme Daudi.
Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.
Ee Yawe, nimesikia juu ya utukufu wako, juu ya matendo yako, nami ninaogopa. Uyafanye tena mambo yale wakati wetu; uyafanye yajulikane wakati huu wetu. Unapokasirika tafazali ukumbuke huruma yako!
Nikaangalia, nami nikaona farasi mwenye rangi ya kijivujivu. Na yule aliyepanda juu yake aliitwa Lufu, naye alikuwa akisindikizwa na Kuzimu. Wao wakapewa uwezo juu ya sehemu moja ya ine ya dunia kwa kuua watu kwa upanga, kwa njaa kubwa, kwa ugonjwa mukali na kwa nyama wakali.
Yawe aliwaua wakaaji makumi saba wa muji wa Beti-Semesi, kwa sababu waliangalia ndani ya Sanduku lake. Watu waliomboleza kwa sababu Yawe alikuwa amefanya mauaji makubwa kati yao.