Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 24:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Halafu, Gadi akamwendea Daudi na kumwelezea, akisema: “Unapendelea njaa ya miaka saba ikuje katika inchi yako? Au wewe uwakimbie waadui zako kwa miezi mitatu wanapokufuatilia? Au kuwe siku tatu ambapo inchi yako itakuwa na ugonjwa mukali? Fikiri unipe jibu nitakalomupa yeye aliyenituma.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 24:13
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati mumoja katika siku za utawala wa Daudi kukatokea njaa kali katika inchi. Njaa hiyo ilidumu miaka mitatu yenye kufuatana. Daudi alimwomba Yawe shauri. Yawe akamwambia: “Saulo na jamaa yake wana makosa ya kumwanga damu kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”


“Kwenda umwambie Daudi hivi: ‘Yawe anasema hivi: Ninakupa mambo matatu, nawe ujichagulie moja kati yao, nami nitakutendea nalo.’ ”


Elisha alikuwa amemwambia mwanamuke aliyeishi Sunemu ambaye alikuwa amemufufua mwana wake: “Ondoka na jamaa yako, uhamie katika inchi ya kigeni kwa sababu Yawe ameleta njaa itakayokuwa katika inchi kwa muda wa miaka saba.”


njaa ya miaka mitatu; au miezi mitatu ya maangamizi kutokana na waadui zako ambapo upanga wa waadui zako utakushinda; au siku tatu ambazo Yawe atawashambulia kwa upanga wake, awaletee ugonjwa mukali katika inchi, na malaika wake apite kuwaangamiza katika inchi nzima ya Israeli. Sasa amua. Ni jibu gani nitakalomupa yeye aliyenituma.’ ”


Hautaogopa ugonjwa mukali unaotokea usiku, wala hasara inayotokea muchana.


Pigo hilo la muto Nili lilidumu siku saba.


Wewe mwanadamu! Taifa fulani likitenda zambi kwa kukosa uaminifu kwangu, mimi nitanyoosha mukono wangu kwa kuliazibu. Nitaiharibu akiba yake ya chakula na kuliletea njaa. Nitawaua watu na nyama wake.


Mutatumia nguvu zenu bure maana mashamba yenu hayatatoa mavuno na inchi yenu haitazaa matunda.


Nitawaletea upanga ambao utalipiza kisasi juu ya agano mulilovunja. Ninyi mutakimbilia katika miji yenu, lakini nitawaletea ugonjwa mukali na kuwatia katika mikono ya waadui zenu.


Ninawaambia ukweli: kulikuwa wajane wengi katika inchi ya Israeli katika siku za nabii Elia. Wakati ule, mvua ilifungwa isinyeshe kwa muda wa miaka mitatu na nusu na kukakuwa njaa kubwa katika inchi yote.


Yawe atawashambulia kwa kifua kikuu, homa, majipu, joto kali, ukavu, zoruba na ukungu; mambo hayo yatawaandama mpaka muangamie.


“Yawe atawafanya mushindwe na waadui zenu. Ninyi mutakwenda kuwashambulia kwa njia moja, lakini mutawakimbia kwa njia saba. Nanyi mutakuwa kinyaa kwa watu wote katika dunia.


Yawe atawapiga kwa majipu yaliyowapata Wamisri, atawapa vidonda, upele na kuwashwa ambavyo hamuwezi kuponywa.


Yawe atashambulia magoti yenu na miguu yenu kwa majipu makali ambayo hamutaweza kuponywa; yatawaenea tangu juu ya kichwa mpaka kwenye vikanyagio vya miguu.


Watu hao watawazunguka katika miji yenu yote, mpaka kuta zenu za makimbilio ambazo mulitegemea zimeporomoshwa chini kila pahali katika inchi yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, amewapa.


Sasa ufikiri juu ya jambo hili na uamue la kufanya. Jambo hili linaweza kuleta hasara kwa bwana wetu na jamaa yake yote. Yeye ni mutu mubaya na hakuna anayeweza kusema naye.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ