Halafu, Gadi akamwendea Daudi na kumwelezea, akisema: “Unapendelea njaa ya miaka saba ikuje katika inchi yako? Au wewe uwakimbie waadui zako kwa miezi mitatu wanapokufuatilia? Au kuwe siku tatu ambapo inchi yako itakuwa na ugonjwa mukali? Fikiri unipe jibu nitakalomupa yeye aliyenituma.”
Yoabu mwana wa Zeruya alianza kuwahesabu lakini hakumaliza; tena kasirani iliwapata Waisraeli kwa ajili ya tendo hili, nayo hesabu haikuingizwa katika kitabu cha habari za mufalme Daudi.
Maana mimi niko pamoja nawe, nipate kukuokoa. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitayaangamiza kabisa mataifa yote, ambayo niliyokusambaza kati yao; lakini sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakuazibu kadiri unavyostahili wala sitakuachilia uende bila kukuazibu. –Ni ujumbe wa Yawe.
Wakati watakapokuwa inje ya inchi yao, inchi hiyo itafurahia Sabato zake hapo itakapokuwa katika hali ya ukiwa. Wakati huo wao watatubu uovu wao wa kuzarau maagizo yangu na kuchukia masharti yangu.