Basi Yawe akamutuma nabii Natani kwa Daudi. Natani alimwendea Daudi, akamwambia: “Kulikuwa wanaume wawili katika muji mumoja. Mumoja alikuwa tajiri na mwingine alikuwa masikini.
Habari za mufalme Daudi toka mwanzo mpaka mwisho juu ya mambo ya utawala wake, uwezo wake, na mambo yaliyomupata yeye, Waisraeli, na falme zote katika inchi zimeandikwa katika vitabu vya nabii Samweli, katika vitabu vya nabii Natani, vilevile katika vitabu vya nabii Gadi.
Mufalme Hezekia alifuata maagizo ambayo Yawe alikuwa amemupa mufalme Daudi kwa njia ya Gadi, nabii wa mufalme na nabii Natani. Hivyo basi, akaweka Walawi katika nyumba ya Yawe, wamoja wao wakiwa na matoazi, wengine vinanda na wengine vinubi. Hiyo ilikuwa amri ya Yawe kwa njia ya manabii wake.
Kisha nabii Gadi akamwambia Daudi: “Usikae hapa katika makimbilio. Ondoka mara moja uende katika inchi ya Yuda.” Basi, Daudi akaondoka, akaenda katika pori la Hereti.
(Hapo zamani katika Israeli kama mutu akitaka kumwomba Mungu shauri, alisema: “Basi, kuja, kuja tuende kwa mwonaji.” Maana mutu anayeitwa nabii siku hizi hapo zamani aliitwa mwonaji).